Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 10:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mimi nitawaimarisha watu wangu, nao watanitii na kuishi kwa kunipendeza. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 10:12
18 Referans Kwoze  

Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Nitawaimarisha watu wa Yuda; nitawaokoa wazao wa Yosefu. Nitawarudisha kwao kwa maana ninawaonea huruma, nao watakuwa kama vile sikuwa nimewakataa. Mimi ni Yawe, Mungu wao, nami nitayasikiliza maombi yao.


Sasa, enyi wazao wa Yakobo, mukuje, tutembee katika mwangaza wa Yawe.


Basi wewe mwana wangu, ukuwe hodari kwa njia ya neema uliyopata katika kuungana kwako na Kristo Yesu.


Mataifa mengine yanafuata njia zao, kwa kuitegemea miungu yao, lakini sisi tunafuata njia zetu kwa kumutegemea Yawe, Mungu wetu, milele na milele.


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Basi kwa sababu mumemukubali Kristo kuwa Bwana wenu, muishi katika kuungana naye.


Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.


Watasema juu yangu: Haki na nguvu viko kwa Yawe peke yake. Wote waliomukasirikia Yawe watakuja kwake na haya.


Lakini yeye akasema: ‘Yawe aliyeniongoza katika maisha yangu, atamutuma malaika wake aende pamoja nawe na kukufanikisha katika safari yako. Nawe utamutwalia mwana wangu muke kutoka kwa jamaa yangu na nyumba ya baba yangu.


Basi kwa kumaliza, musimame imara katika kuungana kwenu na Bwana kwa uwezo wa nguvu zake kubwa.


Kwa hiyo wakubwa wa Yuda wataambiana: “Wakaaji wa Yerusalema wamepata nguvu yao kutoka kwa Yawe wa majeshi, Mungu wao.”


Alikuwa akishirikiana na Mungu, akatoweka, kwa maana Mungu alimupeleka.


Kwa mwisho, wandugu, sisi tumewafundisha namna gani munavyopaswa kuishi kusudi mupate kumupendeza Mungu. Na kweli, ni vile munavyoishi. Na sasa, tunawaomba na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu, muendelee mbele vizuri zaidi katika mwenendo ule.


Sisi tuliwaonya, tuliwafariji na kuwasihi sana muishi sawa inavyomupendeza Mungu, anayewaalika kushiriki naye katika ufalme na utukufu wake.


Nitaitia mikono ya mufalme wa Babeli nguvu na kutia upanga wangu katika mukono wake. Lakini nitaivunja mikono ya Mufalme wa Misri, naye atalalamika mbele ya mufalme wa Babeli kama mutu aliyeumizwa vibaya sana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite