ZAKARIA 10:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Nitawarudisha kutoka inchi ya Misri, nitawakusanya kutoka Asuria; nitawaleta katika inchi ya Gileadi na Lebanoni, nao watajaa kila nafasi katika inchi.
Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.
Waisraeli wanaokuwa katika uhamisho, lile jeshi la Waisraeli, watarizi inchi ya Foinikia mpaka Zerepata. Watu wa Yerusalema wanaokuwa katika uhamisho kule Sefaradi watarizi miji ya Negebu.
Nitawarudisha Waisraeli katika inchi yao, nao watakula mavuno yatakayolimwa juu ya mulima Karmeli na Basani na watatosheka kwa chakula kutoka milima ya Efuraimu na Gileadi.
Yawe anasema hivi juu ya nyumba ya kifalme ya Yuda: Ingawa unaonekana vizuri kama inchi ya Gileadi, kama vichwa vya milima ya Lebanoni, ninaapa kwamba nitakufanya kuwa jangwa, ukuwe muji usiokaliwa na watu.
Anayekuwa jamaa ndogo kati yenu atakuwa kabila, anayekuwa mudogo kuliko wote atakuwa taifa kubwa. Mimi ndiye Yawe; wakati utakapofika nitayatimiza haraka.