Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 10:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nitawarudisha kutoka inchi ya Misri, nitawakusanya kutoka Asuria; nitawaleta katika inchi ya Gileadi na Lebanoni, nao watajaa kila nafasi katika inchi.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 10:10
16 Referans Kwoze  

Watakuja kutoka Misri wakitetemeka kama ndege, wataruka kutoka Asuria kama njiwa nami nitawarudisha kwao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe anasema hivi: Nitawaokoa watu wangu kutoka inchi ya mashariki na kutoka inchi ya magaribi


Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.


Waisraeli wanaokuwa katika uhamisho, lile jeshi la Waisraeli, watarizi inchi ya Foinikia mpaka Zerepata. Watu wa Yerusalema wanaokuwa katika uhamisho kule Sefaradi watarizi miji ya Negebu.


Nitawarudisha Waisraeli katika inchi yao, nao watakula mavuno yatakayolimwa juu ya mulima Karmeli na Basani na watatosheka kwa chakula kutoka milima ya Efuraimu na Gileadi.


Yawe anasema hivi juu ya nyumba ya kifalme ya Yuda: Ingawa unaonekana vizuri kama inchi ya Gileadi, kama vichwa vya milima ya Lebanoni, ninaapa kwamba nitakufanya kuwa jangwa, ukuwe muji usiokaliwa na watu.


Anayekuwa jamaa ndogo kati yenu atakuwa kabila, anayekuwa mudogo kuliko wote atakuwa taifa kubwa. Mimi ndiye Yawe; wakati utakapofika nitayatimiza haraka.


na kuwafanya wakae katika Yerusalema. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nitatawala juu yao kwa uaminifu na haki.


Watanifuata mimi Yawe ninayenguruma kama simba; nitakaponguruma watanifikia toka magaribi wakitetemeka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite