Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Wakati wa usiku, nilimwona malaika akipanda juu ya farasi mwekundu. Malaika yule alikuwa akisimama katika bonde, katikati ya miti ya mihadasi. Nyuma yake kulikuwa farasi wengine wekundu, wa kijivujivu na weupe.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 1:8
26 Referans Kwoze  

Kisha kukatokea farasi mwengine mwekundu. Na yule aliyepanda juu yake akapewa uwezo wa kuondoa amani katika dunia, kusudi watu wauane wao kwa wao. Naye akapewa upanga mukubwa.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Efeso hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeshika nyota saba katika mukono wake wa kuume na anayetembea katikati ya vinara saba vya taa vya zahabu.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Pahali pa miiba kutaota miti ya shindano, na pahali pa michongoma kutaota misunobari. Hilo litakuwa jambo litakalowakumbusha watu juu ya mambo niliyotenda mimi Yawe, kitambulisho cha milele ambacho hakitafutwa.


Nitapanda miti kule katika jangwa: mierezi, mivinje, mijohoro, na mizeituni; nitaweka kule katika jangwa: miberoshi, shindano na misunobari.


Wakati wa maono haya usiku, niliona kiumbe kinachofanana na mwanadamu. Akakuja katika mawingu na kumwendea yule Muzee wa zamani sana. Akakaribishwa mbele yake.


Mimi Danieli niliona maono usiku. Ilikuwa hivi: Upepo ulivuma juu ya bahari kubwa toka pande zote ine za mbinguni.


Halafu Danieli akafunuliwa fumbo hilo usiku katika maono. Naye Danieli akamushukuru Mungu wa mbinguni,


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Ilikuwa usiku wakati watu wanapoota ndoto, wakati usingizi muzito unawashika watu.


Kule Gibeoni, Yawe alimutokea Solomono katika ndoto usiku, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka nami nitakupa.”


Siku moja Yoshua alipokuwa karibu na muji wa Yeriko, aliona kwa rafla mutu mumoja akisimama mbele yake na upanga uliochomolewa katika mukono wake. Yoshua akamwendea, akamwuliza: “Wewe ni wetu au ni wa waadui zetu?”


Lakini Mungu akamufikia Abimeleki katika ndoto usiku, akamwambia: “Wewe utakufa kwa sababu ya mwanamuke uliyemutwaa, maana yuko na mume wake.”


Mupenzi wangu amekwenda katika bustani yake, pahali ambapo miti ya marasi inastawi. Yeye anakulisha kondoo wake na kukusanya mayungiyungi.


Mupenzi wangu ni wangu, nami ni wake. Yeye anakulisha kondoo wake penye yungiyungi.


Niliangalia, nami nikaona farasi mumoja mweupe. Na yule aliyepanda juu yake alikuwa na upindi, akapewa taji. Akatoka akiwa mushindaji na mwenye uwezo wa kuendelea kushinda.


Hivyo wakatangaza katika miji yao yote na kule Yerusalema, wakisema: “Mwende kwenye milima, mulete matawi ya mizeituni, mizeituni ya pori, mihadasi, mingazi na miti mingine kwa kujenga vibanda, kama vile ilivyoandikwa.”


Katika siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kumi na moja, ni kusema mwezi wa Sebati, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yawe lilimufikia nabii Zakaria mwana wa Berekia, mujukuu wa Ido. Zakaria akasema hivi:


Hawa ndio waliotumwa na Yawe kuichunguza dunia.


Hao farasi wakamwambia huyo malaika wa Yawe aliyekuwa akisimama katikati ya miti ya mihadasi: Tumeichunguza dunia yote, nayo kweli imetulia.


Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika: “Niko hapa.”


Kisha Yawe akawaambia: Musikilize maneno yangu, kama kuna nabii kati yenu, mimi Yawe ninajifahamisha kwake katika maono na kuongea naye katika ndoto.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite