Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Babu zenu hawakupata azabu kwa sababu ya kukataa maagizo yangu na amri nilizowapa kwa njia ya watumishi wangu manabii? Wakati huo, wao waligeuka na kusema kwamba: Yawe wa majeshi alikusudia kututendea kulingana na mienendo yetu na matendo yetu, na kweli ndivyo alivyotutendea.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 1:6
46 Referans Kwoze  

Yawe amefanya yale aliyokusudia, ametimiza yale aliyoagiza. Kama alivyopanga tangu kale, ameangamiza bila huruma yoyote. Amewafanya waadui wafurahie azabu yako, amewatukuza mashujaa wa waadui zako.


“Lakini kama hamutaitii sauti ya Yawe, Mungu wenu, kama hamutakuwa waangalifu kushika amri zake zote na masharti ninayowaamuru leo, basi mutapatwa na laana hizi zote:


Mbingu na dunia vitatoweka, lakini maneno yangu hayatabadilika hata kidogo.


Hasira ya Yawe haitatulia, mpaka atakapotimiza na kukamilisha mapenzi ya moyo wake. Kutakuja siku ambapo mutaelewa vema mambo hayo.


Wenye zambi kati ya watu wangu, watakufa katika vita. Hao ndio wanaosema: Hasara haitatufikia wala kutupata!


Ni wachache tu ndio watakaoponyoka katika vita na kurudi kutoka inchi ya Misri na kwenda katika inchi ya Yuda. Halafu Wayuda wote waliobaki kati ya wale waliokwenda kukaa Misri watatambua ni neno la nani lenye nguvu: langu au lao!


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


Lakini ninyi wandugu, hamuko katika giza, kwa hiyo siku ile haitawafikia kwa rafla kama mwizi.


Pale ndipo mutakapotambua tena tofauti inayokuwa kati ya wenye haki na waovu, kati ya mutu anayemutumikia Mungu na asiyemutumikia.


Yawe anasema hivi: Uovu wao wote ulianzia Gilgali; kule ndiko nilipoanza kuwachukia. Kwa sababu ya uovu wa matendo yao, nitawafukuza toka katika nyumba yangu. Sitawapenda tena. Wakubwa wao wote ni waasi.


Kwa hiyo Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Mifupa hiyo ni mufano wa watu wote wa inchi ya Israeli. Wao, wanasema: Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yamepotea nasi tumekwisha kabisa.


Huko ndiko mutakapokumbuka mwenendo wenu na matendo yenu mabaya ambayo yaliwachafua; nanyi mutachukizwa kabisa kwa sababu ya maovu yote muliyotenda.


Lakini Yawe amefanya sawa kwa maana nimeliasi neno lake. Munisikilize enyi watu wote, muyaangalie mateso yangu. Wabinti zangu na vijana wangu wanaume wamepelekwa katika utumwa.


Lakini mujue kwa hakika kwamba mukiniua, mutakuwa mumejiletea laana ninyi wenyewe kwa kumwanga damu isiyokuwa na kosa, na kuleta laana juu ya muji huu na wakaaji wake. Maana, ni kweli kwamba Yawe alinituma niwaambie mambo hayo kusudi muyasikie.


Enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema, mujitahiri, mukiondoa govi za mioyo yenu, mupate kujitoa kwa Yawe. Kama si vile, kasirani yangu itawaka kama moto, nayo itaunguza wala hakuna atakayeizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!


Lakini ninahakikisha ujumbe wa mutumishi wangu, na kukamilisha mipango ya wajumbe wangu. Mimi ndiye ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema, watu watakaa ndani yako tena. Na juu ya miji ya Yuda: Ninyi mutajengwa tena: mabomoko yenu yatatengenezwa tena.


Tafazali mugeuke, kusikuwe uovu; muache sasa, kwa ajili ya haki yangu.


“Hayo yote yatawapata ninyi na kuwaandama mpaka muangamie kwa sababu hamukutii sauti ya Yawe, Mungu wenu, juu ya kushika amri zake na masharti aliyowapa.


“Yawe atawatumia laana, mashaka na kukata tamaa katika shuguli zenu zote mpaka muangamie upesi kwa sababu ya uovu wa matendo yenu na kwa sababu ya kumwacha Yawe.


Nami nitawafanya ninyi kama vile nilivyokusudia kuwafanya wao.


Lakini ninawaonya kwamba musipotimiza ahadi yenu, mutakuwa mumemutendea Yawe zambi; mujue kwa hakika kwamba mutaazibiwa.


Kama mukitii sauti ya Yawe, Mungu wenu, mutapewa baraka hizi:


Wapigapinde wachache kati ya mashujaa wa watu wa Kedari ndio watakaobaki. Ni Yawe, Mungu wa Israeli, anayesema hivyo.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Kwa sababu wao wamesema jambo hilo, sasa nitayafanya maneno niliyokupa wewe Yeremia kuwa moto. Nao watu hawa watakuwa kuni, na moto huo utawateketeza.


Angalia, Wakaldea wamechimba mifereji kuuzunguka muji; wanauzunguka kusudi wapate kuuteka; wanaushambulia. Vita, njaa na magonjwa vitaufanya muji utekwe na watu hao. Kweli mambo uliyotabiri yametokea. Unaona mwenyewe.


Twaa kitabu kingine, uandike maneno yote yaliyokuwa katika kile cha kwanza ambacho Yoyakimu, mufalme wa Yuda, amechoma kwa moto.


Kwenda kwa Ebedimeleki Mwetiopia umwambie hivi: Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Angalia mimi nitatimiza mambo yale niliyosema juu ya muji huo na sio mambo mema. Mambo hayo yatakamilika siku hiyo ukiona wewe mwenyewe.


Nitawaazibu hapahapa mupate kujua kwamba maneno ya hasara niliyosema juu yenu yatatimia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Na hiki kitakuwa kitambulisho chake:


Alipokuwa angali anasema maneno hayo, sauti kutoka mbinguni ikamwambia: Ewe mufalme Nebukadneza, sikiliza ujumbe huu juu yako! Umenyanganywa ufalme!


Siku nitakapotoa azabu, Efuraimu itakuwa kama jangwa! Ninachotangaza kati ya makabila ya Israeli, ni jambo litakalotukia kwa hakika.


Katika siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kumi na moja, ni kusema mwezi wa Sebati, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yawe lilimufikia nabii Zakaria mwana wa Berekia, mujukuu wa Ido. Zakaria akasema hivi:


Basi tukio hilo lilitokana na ahadi ya Yawe kwa mufalme Yehu, kusema: “Wazao wako watatawala Israeli mpaka kizazi cha ine.”


ni vilevile na neno langu mimi: halitanirudilia bila mafanikio, lakini litatimiza mapenzi yangu, litafikia shabaha nililoliwekea.


Mwaka huohuo, katika mwezi wa saba, nabii Hanania akakufa.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninyi mumeona hasara yote niliyouletea Yerusalema na miji yote ya Yuda. Miji hii ni mabomoko mpaka leo wala hakuna mutu anayeishi humo.


Kwa hiyo, kasirani yangu na hasira yangu iliwaka na kumwangika juu ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalema, hata kukakuwa jangwa na mabomoko kama inavyokuwa mpaka leo.


Tulikukosea na kukuasi, nawe haujatusamehe bado.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite