Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 1:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kisha malaika yule akaniambia nitangaze ujumbe huu mwingine: Yawe wa majeshi anasema hivi: Miji yake itafurika tena na fanaka. Yawe atafariji tena Sayuni, atachagua Yerusalema kuwa wake.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 1:17
33 Referans Kwoze  

Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.


Yawe wa majeshi, ambaye kwa utukufu wake amenituma, anasema hivi juu ya mataifa yaliyowakamata mateka watu wake: Hakika, anayewagusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.


Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.


Waisraeli wanaokuwa katika uhamisho, lile jeshi la Waisraeli, watarizi inchi ya Foinikia mpaka Zerepata. Watu wa Yerusalema wanaokuwa katika uhamisho kule Sefaradi watarizi miji ya Negebu.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile nitakapowasafisha ninyi toka maovu yenu yote, nitaifanya miji yenu ikaliwe, nayo mabomoko yajengwe upya.


Kama vile mama anavyomufariji mwana wake, vilevile nami nitawafariji; mutafarijiwa katika Yerusalema.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Mupige kelele za shangwe, enyi mabomoko ya Yerusalema! Yawe amewafariji watu wake, ameukomboa Yerusalema.


Lakini ninahakikisha ujumbe wa mutumishi wangu, na kukamilisha mipango ya wajumbe wangu. Mimi ndiye ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema, watu watakaa ndani yako tena. Na juu ya miji ya Yuda: Ninyi mutajengwa tena: mabomoko yenu yatatengenezwa tena.


Enyi mbingu na dunia, mumusifu Mungu; bahari na vyote vinavyokuwa ndani yenu, mumusifu.


Watu wengine wa Israeli, makuhani na Walawi walikaa katika miji ya Yuda, kila mumoja katika urizi wake.


Lakini kisha nilichagua muji wa Yerusalema ukuwe muji ambamo nitaabudiwa, na nilimuchagua Daudi awatawale watu wangu Waisraeli.’


Mbele ya kuumbwa kwa dunia, Mungu alituchagua kuwa watu wake kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,


Malaika wa Yawe akamwambia yule Shetani: Yawe akulaani, ewe Shetani! Kweli, Yawe aliyechagua Yerusalema akulaani! Huyu ni kama kipande cha kuni kilichoopolewa ndani ya moto!


Nitarudisha hali ya mbele ya watu wangu Waisraeli. Watajenga miji yao iliyoharibiwa na kuishi ndani yake; watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima mashamba na kula mazao yake.


Katika miji ya inchi yenye milima, katika miji ya Shefela na katika miji ya jangwa la Negebu, katika inchi ya Benjamina, kandokando ya Yerusalema na katika miji ya Yuda, watu watahesabu tena kondoo wao. –Ni Yawe anayesema.


Halafu wabinti zao watafurahi na kucheza, vijana na wazee watashangilia kwa furaha. Nitageuza maombolezo yao kuwa furaha, nitawafariji na kuwapa furaha pahali pa huzuni.


Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?


Muimbe kwa furaha, enyi mbingu! Ushangilie ewe dunia, Enyi milima, mulalamike kwa furaha, maana Yawe amewafariji watu wake, anawaonea huruma watu wake wanaoteseka.


Na katika miji mingine, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango na wazao wa watumishi wa Solomono, walikaa katika maeneo yao wenyewe, katika miji yao.


Basi, huyo malaika akaniambia: Tangaza kwa sauti na kusema hivi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Ninasikia wivu sana juu ya Yerusalema na Sayuni.


Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite