Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Lakini nimekasirikia sana mataifa ambayo yanastarehe. Nilikuwa ninayakasirikia kidogo, lakini yaliwaongezea hasara.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 1:15
28 Referans Kwoze  

Nitaiazibu Babeli na wakaaji wote wa Kaldea mukiona kwa macho yenu wenyewe, kwa sababu ya uovu wote walioufanya katika Sayuni. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Hao farasi wakamwambia huyo malaika wa Yawe aliyekuwa akisimama katikati ya miti ya mihadasi: Tumeichunguza dunia yote, nayo kweli imetulia.


Yawe alichukizwa sana na babu zenu.


Kambi zao ziachwe matongo, mutu yeyote asiishi katika mahema yao.


Ole kwenu ninyi munaostarehe kule Sayuni, nanyi munaoishi katika usalama kwenye mulima Samaria! Ninyi munaonekana kuwa waongozi wa taifa kubwa, ambao Waisraeli wote wanawategemea.


Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika!


Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda, siku ile Yerusalema iliponyanganywa; kumbuka maneno haya waliyosema: “Mubomoe Yerusalema! Muongoe hata na misingi yake!”


Tumeshiba muda murefu mazarau ya watajiri, nayo masimango ya wenye kiburi.


Kisha yule malaika aliyeongea nami akaniambia kwa sauti: Wale farasi waliokwenda katika inchi ya kaskazini wameituliza kasirani ya Yawe.


Watu hao wanakata njia yangu, wanazidisha hasara yangu, na hakuna mutu wa kuwazuia.


Lakini wote wanaokuangamiza, wataangamizwa vilevile, na waadui zako wote watapelekwa katika uhamisho; nao wanaokukamata mateka watakamatwa mateka, nao wanaokuwinda, nitawawinda.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Watu wa Israeli wanagandamizwa pamoja na watu wa Yuda. Wale waliokamata mateka wamewabana sana na wanakataa kuwaachilia.


Kwa kasirani ulipita juu ya inchi, uliyakanyaga mataifa kwa hasira yako.


Lakini juu ya wale watu ambao walikuja kupigana na Yerusalema, hizi ndizo hasara ambazo Yawe atawaletea: Miili yao itaoza wangali wazima; macho yao yataoza yakiwa kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza zikiwa katika vinywa vyao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite