Kisha malaika yule akaniambia nitangaze ujumbe huu mwingine: Yawe wa majeshi anasema hivi: Miji yake itafurika tena na fanaka. Yawe atafariji tena Sayuni, atachagua Yerusalema kuwa wake.
Yawe ni Mungu mwenye wivu, anayelipiza kisasi; Yawe analipiza kisasi na ni mwenye kasirani; Yawe analipiza kisasi kwa wapinzani wake, kasirani yake inawaka juu ya waadui zake.
Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.
Utuchungulie kutoka mbinguni, ee Mungu, uone, utuangalie kutoka makao yako matakatifu na matukufu. Iko wapi bidii yako kwa ajili yetu na nguvu yako? Hatuoni tena upendo na huruma yako.
Alivaa haki kama vile nguo ya kujikinga kifua, na wokovu kama kofia ya chuma juu ya kichwa. Alivaa nguo ya kulipiza kisasi, na kujifunika na kanzu ya wivu.
Yawe anajitokeza kama shujaa; kama vile askari katika vita anatatanua kupigana. Anapiga kelele kubwa la vita na kujionyesha mwenye nguvu juu ya waadui zake.
Maana kutakuwa watu watakaobaki kule Yerusalema; kule kwenye mulima Sayuni kutakuwa watu wachache watakaobakia. Yawe wa majeshi amekusudia kukamilisha hayo.
Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.
Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wivu wangu unawaka sana. Nitayaazibu mataifa mengine na hasa watu wa inchi ya Edomu. Wao kwa furaha ndani ya moyo na mazarau walikamata hiyo inchi inayokuwa yangu ikuwe yao.