13 Yawe akamupa yule malaika jibu jema na lenye matumaini.
Yawe anasema hivi: Mutakapopitisha miaka makumi saba huko Babeli, nitawashugulikia na kuitimiza ahadi yangu ya kuwarudisha kwa nafasi hii.
Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.
Yule malaika aliyeongea nami, akanifikia tena, akaniamusha kama vile kumwamusha mutu toka katika usingizi.
Basi, nikamwuliza: Bwana, farasi hawa wana maana gani? Malaika yule aliyesema nami akaniambia: Nitakuonyesha wale farasi wana maana gani.
Niliona mwenendo wao, lakini nitawaponyesha; nitawaongoza na kuwapa faraja, nitawatuliza hao wanaoomboleza.
Nikamwuliza yule aliyesimama upande wa juu wa muto, aliyevaa nguo za kitani: Mambo haya ya kutisha yatadumu mpaka wakati gani?