Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Halafu yule malaika wa Yawe akasema: Ee Yawe wa majeshi, kwa muda gani utaendelea kutokuwa na huruma juu ya muji Yerusalema na miji ya inchi ya Yuda ambayo umeikasirikia kwa muda wa miaka makumi saba?

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 1:12
24 Referans Kwoze  

Uwaambie wakaaji wote wa inchi na makuhani hivi: Kwa muda wa miaka makumi saba iliyopita, ninyi mulikuwa mukifunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba. Munazani mulifunga kwa ajili yangu?


mimi Danieli nilikuwa nikisoma kwa uangalifu vitabu vitakatifu, na humo nikaelewa maana ya jambo lile Yawe alilomufahamisha nabii Yeremia juu ya ile miaka makumi saba, muda ambao utahusika na kuharibiwa kwa Yerusalema.


Yawe anasema hivi: Mutakapopitisha miaka makumi saba huko Babeli, nitawashugulikia na kuitimiza ahadi yangu ya kuwarudisha kwa nafasi hii.


Lakini wewe, ee Yawe, unatawala milele; jina lako linakumbukwa katika vizazi vyote.


Ee Mungu, mpaka wakati gani adui atakuchekelea? Watakufuru jina lako milele?


Watu wale wakalalamika hivi kwa sauti kubwa: “Bwana mutakatifu na mwenye ukweli, mpaka wakati gani utaendelea kungojea kuwahukumu wakaaji wa dunia na kuwaazibu kwa sababu ya kuuawa kwetu?”


Wakati wa usiku, nilimwona malaika akipanda juu ya farasi mwekundu. Malaika yule alikuwa akisimama katika bonde, katikati ya miti ya mihadasi. Nyuma yake kulikuwa farasi wengine wekundu, wa kijivujivu na weupe.


Na hivyo likatimia neno la Yawe alilosema kwa njia ya nabii Yeremia: “Mpaka inchi imetimiza Sabato zake, haitalimwa siku zote itakapokuwa ukiwa mpaka miaka makumi saba itakapotimia.”


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Watu wengi kuliko nywele zangu wananichukia. Wana nguvu sana hao wanaotaka kuniua, hao wanaonishambulia kwa mambo ya uongo. Nirudishe kitu ambacho sikuiba?


Majivu yamekuwa chakula changu, machozi yanachangana na kinywaji changu,


Mpaka wakati gani inchi itaomboleza kwa kukauka, na nyasi za mashamba yote kunyauka? Nyama na ndege wanakufa kwa uovu wa wakaaji wake. Wao wanasema: Mungu hataona mwisho wetu.


Mimi sikuikaa pamoja na wanaojifurahisha, wala sikufurahi pamoja nao. Niliikaa peke yangu nikilemewa na nguvu yako; kwa maana ulinijaza hasira yako.


Yawe anasema hivi: Nitatengeneza upya maisha ya jamaa za wazao wa Yakobo, nitayaonea makao yao huruma; muji wao utajengwa upya kwenye mabomoko yake, nyumba ya kifalme itasimama pahali ilipokuwa mbele.


Nikamwuliza yule aliyesimama upande wa juu wa muto, aliyevaa nguo za kitani: Mambo haya ya kutisha yatadumu mpaka wakati gani?


Ee Yawe, nitakulilia mpaka wakati gani, nawe usinisikilize na kunisaidia? Kwa nini ninalia “Mateso makali!” nawe hautuokoi?


Ee Yawe, utakasirika hata milele? Hasira yako itawaka kama moto hata wakati gani?


wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,


Niliwakasirikia watu wangu, Israeli, nikawafanya watu wangu kuwa wanaharamu. Niliwatia katika mikono yako, nawe haukuwaonea huruma; na wazee uliwabebesha nira nzito sana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite