Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, neno la Yawe lilimufikia nabii Zakaria mwana wa Berekia, mujukuu wa Ido kusema hivi:

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 1:1
17 Referans Kwoze  

tangia kuuawa kwa Abeli mpaka kuuawa kwa Zakaria kwenye hekalu katikati ya mazabahu na Pahali Patakatifu. Kweli ninawaambia: watu wa kizazi hiki watabeba lazima ya mambo hayo yote.


Na hivi mutabeba lazima ya damu iliyomwangwa katika dunia pasipo kosa, tangia kuuawa kwa Abeli aliyekuwa mukamilifu mpaka kuuawa kwa Zakaria, mwana wa Barakia, muliyemwuia kwenye hekalu katikati ya Pahali Patakatifu na mazabahu.


Katika mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Dario, siku ya ine ya mwezi wa kenda, ni kusema mwezi wa Kisileu, neno la Yawe lilimufikia Zakaria.


Katika siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kumi na moja, ni kusema mwezi wa Sebati, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yawe lilimufikia nabii Zakaria mwana wa Berekia, mujukuu wa Ido. Zakaria akasema hivi:


Kazi ya kuijenga upya nyumba ya Mungu katika Yerusalema ilisimama, na hali hiyo ikaendelea mpaka mwaka wa pili wa utawala wa Dario, mufalme wa Persia.


Katika siku ya makumi mbili na ine ya mwezi wa kenda, katika mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yawe wa majeshi lilimufikia nabii Hagai kusema hivi:


Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:


Siku ileile ya makumi mbili na ine, mwezi wa kenda, neno la Yawe lilimufikia Hagai kwa mara ya pili kusema hivi:


katika siku makumi mbili na ine ya mwezi wa sita, mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario.


Wakati ule, manabii wawili, Hagai na Zakaria mwana wa Ido, wakawatolea unabii Wayuda waliokuwa wanakaa Yuda na Yerusalema, katika jina la Mungu wa Israeli.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Neno la Yawe lilifika kwa njia ya nabii Hagai kusema hivi:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite