ZAKARIA 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, neno la Yawe lilimufikia nabii Zakaria mwana wa Berekia, mujukuu wa Ido kusema hivi:
tangia kuuawa kwa Abeli mpaka kuuawa kwa Zakaria kwenye hekalu katikati ya mazabahu na Pahali Patakatifu. Kweli ninawaambia: watu wa kizazi hiki watabeba lazima ya mambo hayo yote.
Na hivi mutabeba lazima ya damu iliyomwangwa katika dunia pasipo kosa, tangia kuuawa kwa Abeli aliyekuwa mukamilifu mpaka kuuawa kwa Zakaria, mwana wa Barakia, muliyemwuia kwenye hekalu katikati ya Pahali Patakatifu na mazabahu.
Katika siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kumi na moja, ni kusema mwezi wa Sebati, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yawe lilimufikia nabii Zakaria mwana wa Berekia, mujukuu wa Ido. Zakaria akasema hivi:
Katika siku ya makumi mbili na ine ya mwezi wa kenda, katika mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yawe wa majeshi lilimufikia nabii Hagai kusema hivi:
Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:
Wakati ule, manabii wawili, Hagai na Zakaria mwana wa Ido, wakawatolea unabii Wayuda waliokuwa wanakaa Yuda na Yerusalema, katika jina la Mungu wa Israeli.