Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 99:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wote wasifu jina lake kubwa la kutisha. Yeye ni mutakatifu!

Gade chapit la Kopi




Zaburi 99:3
20 Referans Kwoze  

Walilalamikiana mumoja kwa mwengine hivi: Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yawe wa majeshi! Dunia yote imejaa utukufu wake.


“Kama musipokuwa waangalifu kwa kushika maneno yote ya sheria hii iliyoandikwa katika kitabu hiki na musipoheshimu na kutukuza jina tukufu la kuogopesha la Yawe, Mungu wenu


Aliwakomboa watu wake na kufanya nao agano la milele. Yeye ni mutakatifu na wa kutisha sana!


Na kila kimoja cha viumbe vya ajabu kilikuwa na mabawa sita yenye kujaa macho ndani na inje. Navyo viliimba muchana na usiku bila kuchoka, vikisema: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwa, anayekuwa na anayekuja.”


Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.


Yawe ni mwenye haki katika njia zake zote; ni mwema katika matendo yake yote.


Mumwambie Mungu: “Matendo yako ni ya ajabu! Kwa nguvu yako kubwa waadui zako wanaishiwa nguvu.


Ukiwa pahali popote unapofanya kazi, mara utakaposikia baragumu, kimbilia kwetu. Mungu wetu atatupigania.”


nikisema: “Ee Yawe, Mungu wa mbinguni, wewe ni Mungu unayekuwa mukubwa na wa kutisha, unashika agano lako na kutenda mema kwa wale wanaokupenda na kushika amri zako.


Lakini Yoshua akawaambia: “Ninyi hamuwezi kumutumikia Yawe, maana yeye ni Mungu Mutakatifu. Yeye ni Mungu mwenye wivu, naye hatawasamehe makosa na zambi zenu.


Basi, musiwaogope, kwa sababu Yawe, Mungu wenu, yuko kati yenu. Yeye ni Mungu mukubwa na wa kutisha.


Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi ya Asafu. Wimbo.


Hakuna anayekuwa mutakatifu kama Yawe; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye; hakuna anayekuwa jiwe la kufichamia kama Mungu wetu.


Lakini wewe Yawe uko pamoja nami. Kwangu wewe ni kama shujaa wa kutisha. Kwa hiyo watesaji wangu watajikwaa, nao hawataweza kunishinda. Watafezeheka kabisa, kwa sababu hawatashinda. Haya yao itadumu hata milele, nayo haitasahauliwa.


Mumutimizie Yawe, Mungu wenu, ahadi zenu; enyi munaokuwa karibu, mumupe zawadi Mungu wa kutisha.


Kwa hiyo, ee Mungu wetu, Mungu mukubwa, mwenye nguvu na wa kutisha, wewe unashika agano lako na kutenda wema. Mateso yaliyotupata, sisi, wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu, manabii wetu, babu zetu na watu wako wote tangu wakati wa wafalme wa Asuria mpaka leo, usiyaone kuwa ni madogo.


Walawi, ni kusema Yesua, Kadimieli, Bani, Hasabuea, Serebia, Hodia, Sebania na Petahia, wakawaambia watu: Musimame na kumusifu Yawe, Mungu wenu. Mumusifu milele na milele! Na watu wakasifu jina lako tukufu, ambalo linatukuka kuliko baraka na sifa zote.


Muingie ndani ya hekalu lake kwa shukrani, muingie katika kiwanja chake kwa kumusifu. Mumushukuru na kulisifu jina lake.


Zaburi ya Daudi. Ee nafsi yangu, umusifu Yawe; nafsi yangu yote isifu jina lake takatifu!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite