2 Yawe ni mukubwa katika Sayuni; ametukuzwa kuliko mataifa yote.
Wewe Yawe ni mukubwa juu ya dunia yote; wewe unatukuzwa juu ya miungu yote.
Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo? Wataambiwa: Yawe ameijenga imara Sayuni, na wamasikini kati ya watu wake watakimbilia kule.
Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.
Yawe anatawala juu ya mataifa yote, utukufu wake unafika juu ya mbingu.
Anatawala milele kwa nguvu yake kubwa; macho yake yanachungulia mataifa yote. Mwasi yeyote asisubutu kumupinga.
Kutoka Sayuni, muji muzuri kupita kipimo, Mungu anajitokeza, akiangaza.
Yawe hajaona ubaya kwa watu wa Yakobo, wala uovu kwa hao watu wa Israeli. Yawe Mungu wao yuko pamoja nao, Yeye anasifiwa kwa vigelegele kati yao, yeye anapokea sifa zao za kifalme.
Maana Yawe, Mungu Mukubwa, anaogopesha. Yeye ni mufalme mukubwa wa ulimwengu wote.
Mumwimbie Mungu mashairi ya sifa; maana yeye ni mufalme wa ulimwengu wote.