Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 99:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe anatawala, mataifa yanatetemeka! Ameikaa juu ya makerubi, nayo dunia inatikisika!

Gade chapit la Kopi




Zaburi 99:1
30 Referans Kwoze  

Yawe anatawala! Furahi, ee dunia! Mufurahi, enyi visanga vingi!


Mimi nitakutana nawe pale. Kutoka juu ya kiti kile cha rehema katikati ya makerubi wale wanaokuwa juu ya Sanduku la Agano, nitazungumuza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.


Umeme wake unaangaza ulimwengu; dunia inauona na kutetemeka.


Yawe anatawala; amejifunika utukufu mukubwa! Yawe amevaa utukufu na nguvu! Ameimarisha ulimwengu, hautatikisika hata kidogo.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo. Zaburi ya Asafu.


wakisema: “Tunakushukuru wewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, unayekuwa na uliyekuwa, kwa maana umetumia uwezo wako mukubwa nawe ukasimika ufalme wako.


Mbingu zikaviringwa na kuwa kama kizingo cha karatasi na kutoweka. Milima yote na visanga vyote vikahamishwa kutoka kwenye nafasi yao.


Basi wapendwa wangu, mulionyesha utii wenu siku zote wakati nilipokuwa kwenu, na sasa ingekuwa vema muendelee kufanya vile katika siku hizi ninapokuwa mbali nanyi. Mutumike kwa ajili ya wokovu wenu kwa woga na kutetemeka,


Na sasa kwa ngambo ya wale waadui zangu walionikataa mimi kuwa mufalme wao, muwalete hapa na kuwaua mbele yangu.’ ”


Lakini wanainchi wenzake walimuchukia. Kwa hiyo wakatuma wajumbe kumufuata nyuma waende kusema: ‘Hatutaki mutu huyu kuwa mufalme wetu.’


Basi akasema: “Mutu mumoja mwenye heshima alifunga safari kwenda katika inchi ya mbali kusudi asimikwe kuwa mufalme na kisha arudie.


Kwa kishindo cha kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka, na kilio chake kitasikilika kati ya mataifa mengine.


Kwa kishindo cha kuanguka kwao, dunia itatetemeka, na kilio chao kitasikilika mpaka kwenye bahari Nyekundu.


Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.


Niliangalia milima, nikaiona ikitetemeka, navyo vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.


Yawe amewamwangia roho ya fujo, wakawapotosha Wamisri katika mipango yao yote, nao wakakuwa kama mulevi anayeyumbayumba akitapika.


Muyaambie mataifa: “Yawe anatawala! Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika. Atahukumu mataifa kama vile inavyofaa.”


Aliinamisha anga, akashuka chini, na wingu jeusi lilikuwa chini ya miguu yake.


“Nimemusimika mufalme niliyemuchagua; anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!”


“Lakini ninyi hamujui wala hamufahamu! Ninyi munatembea katika giza la upotovu! Misingi yote ya haki katika dunia imetikiswa!


Daudi aliondoka pamoja nao wote kuenda Bali-Yuda kwa kuleta Sanduku la Mungu linaloitwa kwa jina la Yawe wa majeshi, anayeikaa kwenye kiti chake cha kifalme juu ya makerubi.


Ee dunia yote; tetemeka mbele yake! Ameweka ulimwengu imara, hautatikisika.


Unitegee sikio, ewe Muchungaji wa Israeli, unayewaongoza wazao wa Yosefu kama kondoo. Ewe unayekaa juu ya makerubi, uangaze,


Mumwabudu Yawe katika pahali pake patakatifu; tetemeka mbele yake, ee dunia nzima!


naye akaniambia: Wewe mwanadamu! Hapa ndipo pahali pa kiti changu cha kifalme, pahali ninapoweka miguu yangu. Nitakaa kati ya watu wa Israeli milele. Na Waisraeli hawatalichafua jina langu, wao wenyewe, wala wafalme wao kwa kuziabudu sanamu au kuzika maiti za wafalme wao pahali hapa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite