mukinitolea mimi Yawe sadaka kutoka katika mifugo yenu, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo au kutoa sadaka ya mapenzi au sadaka ya wakati wa sikukuu zenu zilizowekwa, na kufanya harufu nzuri ya kunipendeza mimi Yawe,
Na muangalie, Mungu mwenyewe ndiye kiongozi wetu na makuhani wake wako na baragumu zao tayari kuzipiga kwa kupana kitambulisho cha kuanza vita juu yenu. Enyi watu wa Israeli, muache kupigana vita na Yawe, Mungu wa babu zenu. Hamuwezi kushinda!”
Walawi wote waimbaji, pamoja na Asafu, Hemani, na Yedutuni, pamoja na Walawi wengine wa ukoo zao, wakiwa wamevaa nguo zao za kitani safi nao wakabeba matoazi, vinanda na vinubi, walisimama upande wa mashariki wa mazabahu. Makuhani mia moja na makumi mbili wapiga baragumu walikuwa pamoja nao.
Hemani na Yedutuni walikuwa na baragumu na matoazi kwa ajili ya muziki na ala za muziki kwa ajili ya nyimbo takatifu. Wana wa Yedutuni walichaguliwa kwa kulinda milango.
Sebania, Yosafati, Netaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, waliokuwa makuhani, waliwekwa kwa kupiga baragumu mbele ya Sanduku la Agano. Obedi-Edomu na Yehiya waliwekwa vilevile kuwa walinzi wa sanduku.
Kwa siku saba mutamufanyia Yawe, Mungu wenu, karamu pahali ambapo Yawe atachagua; kwa sababu Yawe, Mungu wenu atawabariki kwa mazao yenu yote na katika shuguli zenu zote nanyi hakika mutafurahi.
Kwa mwanzo wa kila mwezi, mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.
Amelibomoa hekalu lake kama kibanda katika bustani, ameharibu pahali pake pa kusanyiko. Amefanya sikukuu na siku ya Sabato visahauliwe kule Sayuni, kwa hasira yake kubwa amewakataa mufalme na makuhani.
Alitoa sadaka zile kadiri ilivyotakiwa na amri ya Musa kila siku takatifu, ni kusema siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, na sikukuu tatu za kila mwaka – sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, sikukuu ya majuma na sikukuu ya vibanda.
Daudi aliwaamuru vilevile wakubwa wa Walawi wachague kati ya wandugu zao waimbaji wakuwe wanaimba na kupiga ala za muziki kwa nguvu, kwa kutoa sauti za furaha. Walipiga vinanda, vinubi na matoazi.
Mufalme Daudi na viongozi wa Walawi, wakachagua wazao wa Asafu, wa Hemani, na wa Yedutuni, kwa kuongoza katika kazi ya kutabiri kwa kutumia vinubi, na vinanda na matoazi. Haya ndiyo majina ya wale waliochaguliwa kwa kuongoza ibada, pamoja na aina ya kazi iliyofanywa na kila kikundi: