Maana Yawe anasema hivi: Mushangilie kwa furaha kwa ajili ya Yakobo, mupige vigelegele kwa ajili ya taifa kubwa, mutangaze, musifu na kusema: Yawe ameokoa watu wake, ameleta ukombozi kwa wale waliobaki kati ya Waisraeli!
‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’ ” Yesu akaendelea kuwaambia: “Mungu si Mungu wa waliokufa, lakini ni Mungu wa wanaokuwa wazima.”
‘Mumwambie Yosefu kwa ajili yangu: Tafazali uwasamehe wandugu zako makosa yao mabaya na maovu yote waliyokutendea.’ Sasa basi, tafazali usamehe uovu tuliokutendea sisi watumishi wa Mungu wa baba yako.” Yosefu alipopata ujumbe huu, akalia.
Walifanya kazi yao ya kuimba mbele ya hema takatifu la mukutano mpaka wakati mufalme Solomono alipojenga hekalu la Yawe kule Yerusalema. Walitumika kazi yao vizuri kufuatana na zamu ya kila kundi.