Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 127:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Wimbo wa safari za kidini: wa Solomono. Yawe asipoijenga nyumba, wanaoijenga wanajisumbua bure. Yawe asipoulinda muji, wanaoulinda wanakesha bure.

Gade chapit la Kopi




Zaburi 127:1
35 Referans Kwoze  

Mutu anaweza kufanya mipango yake, lakini Yawe anaongoza hatua zake.


Hivi yule anayepanda na yule anayenyweshea maji, wote si kitu; Mungu ndiye anayekuwa wa lazima kwa maana ni yeye anayeotesha mbegu.


Wimbo wa safari za kidini. Ninyi wote munaokuwa katika Israeli museme: “Kama Yawe asingalikuwa upande wetu”.


Juu ya kuta zako, ee Yerusalema, nimeweka walinzi, usiku na muchana hawatakaa kimya hata kidogo. Enyi munaomukumbusha Yawe ahadi yake, musikae kimya;


Basi fanya angalisho na kukumbuka kwamba Yawe amekuchagua wewe umujengee nyumba ya ibada. Ukuwe hodari na utende hivyo.”


Mupandishe bendera ya vita kwa kushambulia kuta za Babeli. Muimarishe walinzi, muweke walinzi, mutayarishe mashambulizi. Yawe amepanga na kutimiza mambo aliyosema juu ya wakaaji wa Babeli.


Kisha, mufalme Daudi akamwambia Solomono mwana wake: “Uwe imara na hodari, ufanye kazi hii. Usiogope wala kuwa na wasiwasi. Yawe Mungu ambaye ni Mungu wangu, yuko pamoja nawe. Hatakuachilia lakini atakuwa nawe mpaka itakapomalizika kazi yote ambayo inayohitajika kufanyiwa kwa nyumba ya Yawe.


Na kama Kristo hakufufuka, mahubiri yetu ni ya bure na kuamini kwenu ni kwa bure vilevile.


Wimbo wa safari za kidini. Ninainua macho kwenye milima. Musaada wangu unatoka wapi?


Wimbo wa safari za kidini. Ninainua macho kwako, ee Yawe, wewe unayeikaa huko juu mbinguni!


Wimbo wa safari za kidini. Katika taabu yangu nilimwita Yawe, naye akanijibu.


Wimbo wa safari za kidini. Wanaomutegemea Yawe, wako kama mulima Sayuni, ambao hautikisiki lakini unabaki imara siku zote.


Alijenga hapo hekalu lake kubwa kama mbingu, kama dunia aliyoiimarisha milele.


Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu; wote hawana akili yoyote. Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka, wanalala tu na kuota ndoto, wanapenda sana kusinzia!


Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja.


Wimbo wa safari za kidini. Yawe alipoturudisha tena Sayuni, tulikuwa kama watu wanaoota ndoto!


Wimbo wa Safari za kidini. Wa Daudi. Nilifurahi waliponiambia: “Twende kwenye nyumba ya Yawe.”


Mimi, Yawe, ni mulimaji wake; ninalimwangilia maji kila wakati. Ninalilinda usiku na muchana, kusudi lisiharibiwe na mutu yeyote.


Umujalie Solomono mwana wangu kusudi kwa moyo wote ashike amri zako, ushuhuda na maagizo yako, atimize yote na apate kujenga nyumba hii ya utukufu niliyoifanyia matayarisho.”


Ninawaogopea, kwa maana inawezekana kwamba nimesumbuka bure kwa ajili yenu!


Walinzi wa muji walinikuta, walipokuwa wakizunguka katika muji. Wakanipiga na kuniumiza; nao walinzi wa mulango wakaninyanganya ushungi wangu.


Walinzi wa muji waliniona walipokuwa wanazunguka katika muji. Basi nikawauliza: Mumemwona mupenzi wangu wa moyo?


Wakimbiaji wanakimbia wakitoleana ujumbe mumoja kwa mwingine kwa kumupasha mufalme wa Babeli habari kwamba muji wake umeshambuliwa kila upande.


Zaburi ya Solomono. Ee Mungu, umujalie mufalme uwezo wa kufuata sheria yako, umupe mwana wa mufalme haki yako.


Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye anayewapa uwezo wa kupata utajiri. Anafanya hivyo kwa kuimarisha agano alilofanya na babu zenu mpaka leo.


Mufalme wa muji wa Yeriko akaambiwa: “Wanaume wawili Waisraeli wameingia katika muji leo usiku kwa kuipeleleza inchi.”


Alitunga mezali elfu tatu na nyimbo elfu moja na tano.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite