Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 102:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Siku zangu zinapita kama moshi; mifupa yangu inaungua kama katika furu.

Gade chapit la Kopi




Zaburi 102:4
21 Referans Kwoze  

Majani yananyauka na maua yanafifia, Yawe anapovumisha upepo juu yake. Hakika wanadamu ni kama majani.


Maana hao watatoweka mara moja kama nyasi; watanyauka kama majani.


Wakati wa taabu ninamutafuta Bwana wetu; ninamunyooshea mikono yangu usiku bila kuchoka, lakini sifarijiwi na mutu yeyote.


Kisha, Ezra akaondoka mbele ya nyumba ya Mungu, akaenda kwa nyumba ya Yehohanani mwana wa Eliasibu. Kule, Ezra akalala usiku kucha bila kula wala kunywa maji, kwa huzuni aliyokuwa nayo juu ya ukosefu wa imani ya watu waliotoka katika uhamisho.


Akabaki muda wa siku tatu pasipo kuona, naye hakukula wala kunywa kitu.


Ninafikiri juu ya hayo siku zote, nayo roho yangu imejaa huzuni.


Alinichoma ndani ya moyo kwa mishale, kutoka katika kifuko chake.


kwa sababu ya kasirani na hasira yako, maana umeniokota na kunitupilia mbali.


Muchana kutwa waadui zangu wananisimanga, wanaonichekelea wanatumia jina langu kwa kulaani.


Wewe unajua ninavyotukanwa, unajua haya na matusi ninazopata; na waadui zangu wote wewe unawajua.


Mbona ninaugua hivyo katika moyo? Kwa nini ninahangaika hivyo ndani yangu? Nitamutumainia Mungu, maana nitamusifu tena yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.


naye anapoteza hamu yote ya chakula, hata chakula ni chukizo kwake.


Ninachukia maisha yangu! Malalamiko yangu nitayasema bila kizuizi. Nitasema kwa uchungu wa moyo wangu.


Mishale ya Mungu Mwenye Uwezo imenichoma; nafsi yangu imekunywa sumu yake. Vitisho vya Mungu vimenipata.


Wazee wa nyumba yake walimufuata na kumusihi aamuke, lakini yeye alikataa, na hakukula chakula chochote pamoja nao.


Ngozi yangu inakuwa nyeusi na inachubuka, mifupa yangu inaungua kwa homa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite