Kisha, Ezra akaondoka mbele ya nyumba ya Mungu, akaenda kwa nyumba ya Yehohanani mwana wa Eliasibu. Kule, Ezra akalala usiku kucha bila kula wala kunywa maji, kwa huzuni aliyokuwa nayo juu ya ukosefu wa imani ya watu waliotoka katika uhamisho.
Mbona ninaugua hivyo katika moyo? Kwa nini ninahangaika hivyo ndani yangu? Nitamutumainia Mungu, maana nitamusifu tena yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.