Usinigeuzie mugongo, usinikatae kwa hasira mimi mutumishi wako. Wewe umekuwa siku zote musaada wangu. Usinitupe wala usiniachilie, ee Mungu Mwokozi wangu.
Majaribu yale munayopata, ni yale yanayowapata watu wengine wote. Mungu hatawaachilia kujaribiwa kupita nguvu zenu, kwa maana yeye ni mwaminifu. Jaribu litakapowatokea, atawapatia nguvu ya kulivumilia, hata muweze kulishinda.
Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.