Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 102:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Maombi ya mutu anayekuwa katika taabu ambaye anamutolea Yawe malalamiko yake.

Gade chapit la Kopi




Zaburi 102:1
28 Referans Kwoze  

kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya kifo ilikuwa mbele yangu.


Usikie kilio changu, ee Mungu, usikilize maombi yangu.


Unapomwazibu mutu zambi zake kwa kumwadibisha, unaharibu kama nondo kile anachokipenda. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Nyuma ya muda murefu, mufalme wa Misri akakufa. Waisraeli wakaugua na kulia kutokana na hali yao ya utumwa na kilio chao kikamufikia Mungu juu.


Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


Yesu alikuwa katika uchungu mukubwa, akazidi kuomba kwa bidii. Jasho iliyomutoka ikakuwa kama matone ya damu yaliyokuwa yakitiririka mpaka chini.]


Umejifunika wingu kusudi maombi yoyote yasipite.


Ingawa ninaita na kuomba musaada anazuiza maombi yangu yasimufikie.


Ee Yawe, unijibu haraka; maana roho yangu imeregea kabisa! Usinigeuzie mugongo, kusudi nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.


Roho yangu imeregea kabisa; moyo wangu unaugua.


Ee Yawe, usikilize maneno yangu, usikie malalamiko yangu.


Kisha, makuhani na Walawi wakawaombea watu baraka za Yawe, naye katika makao yake matakatifu kule mbinguni akasikia maombi yao na kuyakubali.


“Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mutu kutoka inchi ya kabila la Benjamina, nawe utamupakaa mafuta kuwa mutawala wa watu wangu Waisraeli. Yeye atawaokoa watu wangu kutoka kwa Wafilistini, maana nimeyaona mateso ya watu wangu na kilio chao kimenifikia.”


Kisha wakaitupilia mbali miungu ya kigeni, wakamutumikia tena Yawe. Yawe hakuweza kuvumilia zaidi kuona taabu za Waisraeli.


Anajibia mahitaji yao wote wanaomwabudu; anasikia kilio chao na kuwaokoa.


Wakati wa taabu ninamutafuta Bwana wetu; ninamunyooshea mikono yangu usiku bila kuchoka, lakini sifarijiwi na mutu yeyote.


Wokovu na utukufu wangu vinatoka kwa Mungu; kikingio changu chenye nguvu na kimbilio langu ni Mungu.


Machozi ni chakula changu muchana na usiku; ninaambiwa kila siku: “Mungu wako yuko wapi?”


Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite