Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 101:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Nitateketeza yule anayemuteta mwenzake, sitamuvumilia mwenye majivuno na kiburi.

Gade chapit la Kopi




Zaburi 101:5
25 Referans Kwoze  

bila kosa kwa wale ambao hawafanyi makosa, lakini mukali kwa waovu.


Kuna watu ambao macho yao yanajaa kiburi. Wanazarau kila kitu wanachoona.


Unaikaa kitako kumuteta mwanadamu mwenzako, unamuchongea ndugu yako wa tumbo.


Vilevile uwaambie wanawake wazee wakuwe na mwenendo unaostahili kwa watu watakatifu. Hawapaswi kuwa wasingiziaji, wala wasikuwe watumwa wa pombe, lakini wakuwe wenye kutoa mafundisho mazuri.


Lakini niliwaandikia kwamba musishirikiane na mutu anayejiita ndugu mwamini, akiwa mwasherati, mwenye tamaa, mwenye kuabudu sanamu, mutukanaji, mulevi au munyanganyi. Na zaidi ya ile musichangie chakula na mutu wa namna hii.


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Mupiga domo hafichi siri. Kwa hiyo umwepuke mutu wa kusemasema.


Kwako kuna wanaowasingizia wengine kusudi wauawe. Wakaaji wako wanashiriki chakula kilichotolewa kwa miungu juu ya milima. Watu wako wanatenda uasherati.


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Upepo wa kaskazini unaleta mvua; vilevile mwenye kusingiziana analeta chuki.


Anayemuchukia mwingine kwa siri ni munafiki. Anayemusingizia mutu ni mupumbafu.


Ee Yawe, ingawa wewe uko juu ya wote, unawaangalia wanyenyekevu kwa wema; lakini, unatambua wenye kiburi kwa mbali.


Muache kujisifu, muache kusema kwa kiburi. Maana anayejua ni Yawe. Yeye anayapima matendo yote.


Usipitepite hata kidogo ukiwachongea watu wa jamaa yako. Usitie maisha ya mwenzako katika hatari ya kifo kwa maneno yako. Mimi ni Yawe.


Usitoe habari za uongo. Usishirikiane na mutu mwovu kwa kuwa mushuhuda mubaya.


Usimushuhudie mwenzako uongo.


Wanawake wao wanapaswa kuwa na adabu vilevile, wasikuwe wasingiziaji wa uongo, lakini wakuwe wakadirifu na waaminifu katika mambo yote.


Macho ya kiburi na moyo wa majivuno vinaonyesha wazi zambi ya waovu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite