Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 101:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 sitavumilia hata kidogo mambo ya upuuzi. Ninachukia matendo ya watu wapotovu, mimi sitaambatana nayo.

Gade chapit la Kopi




Zaburi 101:3
44 Referans Kwoze  

Uniepushe nisifuate mambo ya ovyo; unionyeshe njia yako, unipe uzima.


Nimejizuiza kabisa mimi mwenyewe, macho yangu yasimwangalie binti kwa tamaa.


Usimutamani mwanamuke yule kwa uzuri wake, wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemwangalia mwanamuke kwa kumutamani, amekwisha kuzini naye ndani ya moyo wake.


Alinifundisha wimbo mupya, wimbo wa sifa kwa Mungu wetu. Wengi wataona, wataogopa, na kisha watamutumainia Yawe.


Usitamani nyumba ya mwenzako, wala muke wake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.


Muangalie wazo ovu lisiwaingie ndani ya mioyo yenu, mukisema: ‘Mwaka wa saba, mwaka wa kusamehe wadeni uko karibu’. Mukimwangalia ndugu yenu masikini na jicho baya na kukataa kumupa chochote, yeye anaweza kumulilia Yawe juu yenu na hiyo itakuwa zambi kwenu.


Maana ingekuwa heri kwao kama wasingejua njia ya haki, kuliko kuijua na kisha kuacha ile amri takatifu waliyopewa.


Lakini sasa munamujua Mungu, au afazali tuseme kwamba sasa munajulikana naye. Basi namna gani mumerudilia tena vitu vinavyotawala dunia, visivyokuwa na uwezo na vikosefu, mukitaka kuwa watumwa tena?


Upendo wenu ukuwe pasipo udanganyifu. Muchukie chochote kinachokuwa kibaya, mushikamane na kinachokuwa chema.


Lakini macho yako wewe na moyo wako, vinaelekea tu mapato yasiyokuwa ya haki. Unamwanga damu ya wasiokuwa na kosa, nawe unawatesa watu na kuwatendea kwa ukali.


Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kumata upepo. Afazali kufurahia kitu ambacho uko nacho kuliko kuhangaika kwa kutamani kitu kingine.


Kwa hiyo, mukuwe imara katika kushika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa, musiyaache hata kidogo.


Lakini sisi si watu wenye kurudi nyuma na kupotea, lakini sisi ni watu wenye imani na wenye kuokoka.


Ninachukia watu wanafiki, lakini ninapenda sheria yako.


Walimujaribu Mungu tena na tena, wakamukasirikisha huyo Mutakatifu wa Israeli.


Lakini wote wamekosa, wote wamepotoka pamoja; hakuna anayetenda mazuri, hakuna hata mumoja.


Wameacha mara moja njia niliyowaamuru, wakajifanyia sanamu ya mwana-ngombe, nao wamemwabudu na kumutolea sadaka wakisema: Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa katika inchi ya Misri!


Wanatamani mashamba na kuyatwaa; wakitaka nyumba, wananyanganya. Wanawatesa wenye nyumba na jamaa zao, wanawanyanganya watu mali zao.


Ni mutu anayekuwa hivi: anaishi kwa haki na kusema kwa usawa, anazarau kabisa utajiri wa unyanganyi, anakataa kupokea kituliro, hakubali hata kidogo kusikia mipango ya mauaji, wala hakubali macho yake yaone maovu.


Mugeuke na kuiacha njia ya ukweli; musituambie tena juu ya Mungu, Mutakatifu wa Israeli.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.


Lakini wanaogeuka na kufuata njia zao mbaya, uwatoweshe pamoja na watenda maovu. Amani ikuwe na Israeli!


Yawe anawapenda wale wanaochukia uovu, anayalinda maisha ya watu wake, anawaokoa kutoka makucha ya waovu.


Lakini waligeuka na kufanya mabaya kama babu zao; wakayumbayumba kama upinde usiokuwa imara.


Mwovu anajipendelea mwenyewe, anafikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa.


“Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.


Mutakusanya vitu vyote mulivyoteka katika kiwanja cha muji na kuchoma kwa moto vitu vile vyote kama vile sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yawe, Mungu wenu. Muji huo utakuwa lundo la mabomoko milele, nao hautajengwa tena.


Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.


Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua; hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”


Waadui zako ni waadui zangu; ninawachukia kabisa kabisa.


Mutu mwovu, mutu asiyefaa kitu, anatangatanga akisema maneno mapotovu.


Anakonyeza jicho kwa kuwakosesha wengine, anaparuza kwa miguu na kufanyia watu kitambulisho kwa vidole.


Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.


Mutu yeyote asikusudie kumutendea mwenzake ubaya wala musiape uongo, maana ninayachukia sana matendo hayo. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite