Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 101:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Nitashikamana na mwenendo mukamilifu. Utakuja kwangu wakati gani? Nitaishi kwa ukamilifu ndani ya nyumba yangu;

Gade chapit la Kopi




Zaburi 101:2
22 Referans Kwoze  

Nimeapa na kuhakikisha kiapo changu, kwamba nitashika maamuzi yako ya haki.


Nawe kama ukinitumikia kwa ukamilifu wa moyo na usawa kama baba yako Daudi alivyofanya, ukitii amri zangu na kutimiza yale yote niliyokuamuru, ukifuata masharti yangu na maagizo yangu,


Muondoke kwangu, enyi waovu, kusudi nipate kushika amri za Mungu wangu.


Nitawaangalia waaminifu katika inchi, wapate kuishi pamoja nami. Watu wakamilifu, ndio watakaonitumikia.


Lakini wanaokutafuta wafurahi na kushangilia. Wanaopenda uwaokoe waseme siku zote: “Yawe ni mukubwa!”


Maana, alipokuwa muzee, wake zake walimupotosha hata akaitumikia miungu mingine, wala hakukuwa mwaminifu kabisa kwa Yawe, Mungu wake, kama baba yake Daudi alivyokuwa mwaminifu.


na kuwafundisha kwa uangalifu watoto wenu. Mutawaelezea mutakapokuwa munakaa katika nyumba au munapokuwa katika safari au munapolala au munapoamuka.


Nguvu za Mungu zilikuwa zikifanya kazi katika Yuda, zikitia moyo wa kutii amri za mufalme na wakubwa wake kadiri ya maagizo ya Yawe.


Lakini hata hivyo pahali pa kutambikia miungu mingine katika Israeli hapakuharibiwa; lakini yeye alikuwa na moyo mwaminifu maisha yake yote.


Ahimeleki akamujibu: “Kati ya watumishi wako, Daudi ndiye mukubwa wa kuaminika kuliko wote. Yeye ni mukwe wako wewe mufalme mwenyewe, mukubwa wa waaskari wako walinzi na anaheshimiwa kuliko wote katika nyumba yako.


Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”


Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”


akisema: Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote, na kutenda mazuri mbele yako. Hezekia akalia kwa uchungu sana.


Kwa hiyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akawahukumu watu wake wote kufuatana na haki na sheria.


Ninyi mutanijengea mazabahu ya udongo. Juu yake mutanitolea kondoo wenu na ngombe wenu kama sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Pahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, pale pale mimi mwenyewe nitawafikia na kuwabariki.


Lakini mimi ninaishi katika ukamilifu; unihurumie na kunikomboa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite