Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki hata kidogo. Anafanikiwa katika yote anayofanya.

Gade chapit la Kopi




Zaburi 1:3
32 Referans Kwoze  

Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya maji, unaopenyeza mizizi yake karibu na chemichemi. Hauogopi wakati wa jua kali, majani yake yanabaki mabichi. Hauhangaiki katika mwaka wa ukosefu wa mvua, nao haukosi kuzaa matunda.


Kisha kwa ukingo wa muto huo kutaota kila namna ya miti inayotoa chakula. Majani yake hayatanyauka wala miti hiyo haitaacha kuzaa matunda. Itazaa matunda mapya kila mwezi, kwa sababu inapata maji yanayotiririka kutoka hekalu la Mungu. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatatumika kwa kuponyesha magonjwa.


Kama miti iliyopandwa katika nyumba ya Yawe, wanastawi katika viwanja vya Mungu wetu;


Kama mutu asipokaa ndani yangu, yeye ni kama tawi linalotupwa na kukauka. Matawi yanayokauka yanakusanywa na kutupwa katika moto nayo yanateketea.


Mama yako alikuwa kama muzabibu katika shamba, uliopandikizwa pembeni ya maji, ambao ulizaa sana kwa kuwa na maji mengi.


Yule mukubwa wa kifungo hakujishugulisha tena na kitu chochote Yosefu alichopewa kwa maana Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kufanikisha kila kitu alichofanya.


Muto ule ulitelemuka katikati ya barabara ya muji mutakatifu. Kandokando ya ule muto, kulikuwa kumeota muti wa uzima, nao unatoa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, maana yake mara moja kila mwezi. Majani ya muti ule yanatumiwa kama dawa ya kuponyesha mataifa.


Muzabibu ulikuwa umepandikizwa penye udongo muzuri na karibu na maji mengi, kusudi upate kutoa matawi na kuzaa matunda uweze kuwa muzabibu muzuri sana!


Wakati jua lilipokuwa kali, likazichoma, na kwa sababu hazikukuwa na mizizi mikubwa, zikakauka.


Kila kazi aliyoifanya katika utumishi wa nyumba ya Mungu au katika kutii sheria na amri za Mungu kwa kufuata uongozi kutoka kwake, alizifanya kwa moyo wake wote, naye akafanikiwa.


Yule bwana wake akatambua kwamba Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, na kwamba ndiye aliyefanikisha mambo yote Yosefu aliyofanya.


Utapata matunda ya jasho lako, utafurahi na kupata uheri.


Muwaambie watu wa haki jinsi wanavyokuwa na heri, maana watakula matunda ya matendo yao.


Watachipuka kama nyasi penye maji mengi, kama majani kandokando ya vijito.


lakini kwa harufu tu ya maji utachipuka, utatoa matawi kama chipukizi.


Wakati siku za mavuno zilipotimia, akawatuma watumishi wake kwa wale walimaji kusudi wamupatie sehemu yake ya mavuno.


Akaona muti wa tini pembeni ya njia, akaenda karibu nao, lakini hakuona kitu juu yake isipokuwa majani matupu. Halafu Yesu akaulaani muti ule akisema: “Wewe usitoe tena matunda tangu leo hata milele!” Na pale pale muti ule ukakauka.


Kufika kwao kunaleta machafuko katika karamu zenu za upendo. Wanakula na kushiba pamoja nanyi pasipo haya yoyote. Wao ni kama mawingu yanayopeperushwa na upepo pasipo kuleta mvua. Wao ni kama miti isiyozaa matunda hata wakati wa mavuno; ni miti iliyoongolewa na kufa kabisa.


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Nao wakamujibu: “Atawaua hao watu wabaya pasipo huruma, naye atapatana na walimaji wengine kwa kutunza shamba lake na kumupatia sehemu yake ya matunda kwa wakati wa mavuno.”


“Sasa, mwana wangu, Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe kusudi uweze kumujengea nyumba kama vile alivyosema.


Naye anayepita karibu asiwaambie: “Yawe awabariki! Tunawabariki kwa jina la Yawe!”


Watu wengi sana walikuja wakamuletea Yawe sadaka kule Yerusalema, vilevile wakamuletea Hezekia, mufalme wa Yuda zawadi za bei kali. Hivyo kutoka wakati ule, akasifiwa sana na mataifa mengine yote.


Ni kama mabonde yanayotiririka maji, kama bustani kandokando ya muto, kama miti ya mishubiri Yawe aliyopanda, kama mierezi kandokando ya maji.


Baraka za Yawe zitakuwa katika gala zenu za ngano na katika shuguli zenu zote. Atawabariki katika inchi ambayo anawapa.


Basi, Yawe alikuwa pamoja naye, na alimwezesha kwa kila jambo alilotenda. Alimwasi mufalme wa Asuria na kukataa kumutumikia.


Ukiwa mwangalifu, na ukitii masharti na maagizo ambayo Yawe alimwagiza Musa juu ya Israeli, utastawi. Ujipe moyo, ukuwe imara. Usiogope wala usifazaike.


Neno lolote utakalokusudia litafanikiwa, na mwangaza utaangazia njia zako.


inaendelea kuzaa matunda hata katika uzee; siku zote wamejaa utomvu na wabichi,


Mimi Yawe nitawaongoza siku zote, nitatimiza mahitaji yenu wakati wa shida. Nitawaimarisha katika mwili, nanyi mutakuwa kama bustani iliyomwangiliwa maji, kama chemichemi ya maji ambayo maji yake hayakauki hata kidogo.


Kwa hiyo, ulirefuka sana kupita miti yote katika pori; matawi yake yalizidi kuwa mengi na makubwa, kutokana na maji mengi ndani ya mizizi yake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite