Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 lakini anafurahia sheria ya Yawe, na kuifikiri muchana na usiku.

Gade chapit la Kopi




Zaburi 1:2
24 Referans Kwoze  

Hakikisha kwamba hautakisahau hata kidogo kitabu hiki cha sheria; lakini kila siku utajifunza kitabu hiki, muchana na usiku, kusudi upate kutimiza yote yaliyoandikwa humu, nawe utastawi na kufanikiwa.


Kama sheria yako isingekuwa furaha yangu, ningalikwisha kuangamia kwa taabu zangu.


Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.


Ndani ya roho yangu ninapendezwa na Sheria ya Mungu,


Palepale maneno yako yaliponifikia, niliyameza; nayo yakanifurahisha, yakakuwa matamu katika moyo wangu, maana mimi ninajulikana kwa jina lako, ee Yawe wa majeshi.


Uniongoze katika njia ya amri zako, maana humo ninapata furaha yangu.


Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.


Upendezwe na hayo mashairi yangu, ee Yawe, maana wewe ndiye furaha yangu.


Halafu nikasema: “Ninakuja. Katika kitabu imeandikwa juu yangu.


Heri watu wanaoishi katika ukamilifu, wanaofuata sheria ya Yawe.


Kwa maana kumupenda Mungu ni kutii amri zake. Na amri zake si ngumu,


Sijaacha hata kidogo kushika amri yake; maneno yake nimeyatunza ndani ya moyo wangu.


Ufikiri sana juu ya mambo hayo na ujitolee kwa kuyatimiza hata watu wote waone waziwazi maendeleo yako.


Sheria uliyoweka ni bora kwangu, kuliko mali zote za dunia.


Kisha akabaki mujane, hata akaeneza umri wa miaka makumi nane na mine. Alibaki katika hekalu, akitumikia Mungu usiku na muchana, akifunga kula chakula na kuomba.


Ninamushukuru Mungu ambaye ninamutumikia kwa zamiri safi kama vile babu zangu walivyofanya, ninapokukumbuka siku zote katika maombi yangu usiku na muchana.


Wandugu, munakumbuka namna tulivyosumbuka na kazi ngumu. Wakati tulipowahubiria Habari Njema ya Mungu, tulitumika muchana na usiku kusudi tusimulemee hata mutu mumoja kati yenu.


Basi, Mungu hatawapatia haki wale wachaguliwa wake wanaomulilia usiku na muchana? Au atakawia kuwasaidia?


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora: Kwa mutindo wa wimbo wa huzuni. Mashairi ya Hemani Mwezra.


Siku moja magaribi, Isaka akakwenda kwenye mashamba kwa kufikiri. Basi, akainua macho akaona ngamia wanakuja.


Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza Sheria ya Yawe, kuitii na kuwafundisha watu wa Israeli masharti na maagizo zake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite