Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zaburi 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;

Gade chapit la Kopi




Zaburi 1:1
52 Referans Kwoze  

Anayeandamana na wenye hekima anapata hekima, lakini anayejiunga na wapumbafu atapata hasara.


Mimi sikuikaa pamoja na wanaojifurahisha, wala sikufurahi pamoja nao. Niliikaa peke yangu nikilemewa na nguvu yako; kwa maana ulinijaza hasira yako.


Lakini Yesu akajibu: “Heri zaidi wale wanaosikia neno la Mungu na kulitii!”


Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki; lakini njia ya waovu itaangamia.


Wewe mwana wangu usiandamane nao, uzuie muguu wako usifuatane nao.


Malaika wa Yawe anawalinda wote wanaomwabudu, na kuwaokoa kutoka katika hatari.


Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.


Kila anachosema ni uovu na uongo; ameacha kutumia hekima na kutenda mema.


Kufanikiwa kwao si kuko katika mikono yao, wakiwa wamemuweka Mungu mbali na mipango yao?


Kwa hiyo sasa mutwae silaha zote Mungu anazowapatia. Kwa njia hii mutaweza kushinda adui yenu siku mbaya itakapowafikia. Nanyi mutakapokwisha kumaliza mapigano, mutaweza kusimama imara.


lakini mimi sitashiriki mashauri yao mabaya. Ee roho yangu, usishiriki mikutano yao, maana, katika hasira yao, walimwua mutu, kwa mapenzi yao walikata mushipa wa ngombe.


Abarikiwe mutu anayenitegemea mimi Yawe, mutu ambaye mimi Yawe ndiye tegemeo lake.


Kuwa na akili kunaleta ukubali, lakini njia ya waovu ni ya taabu.


Muondoke kwangu, enyi waovu, kusudi nipate kushika amri za Mungu wangu.


Heri wale wanaofuata sheria ya Mungu, wanaotenda siku zote mambo ya haki.


Mimi nimesimama pahali penye kuwa imara; nitamusifu Yawe katika kusanyiko kubwa.


vitakuepusha na njia ya uovu, na watu wa maneno mapotovu,


“Lakini watu wangu hawakunisikiliza; Israeli hakunitaka kabisa.


Lakini njia ya waovu ni kama giza nene, hawajui kinachowafanya wajikwae.


Yeye anazarau wenye mazarau, lakini anakubali wanyenyekevu.


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


Kama una hekima, itakufaa wewe mwenyewe; kama ukiizarau, wewe mwenyewe utapata hasara.


Yawe Mungu ni jua na ngao yetu. Anatukubali na anatupatia utukufu. Hawanyimi kitu chochote kizuri wale wanaoishi katika ukamilifu.


Kwa njia ya imani, Yesu ametuwezesha kukaribia neema ya Mungu, inayokuwa musingi wetu. Sababu hii tunafurahi tukiwa na tumaini la kushiriki katika utukufu wa Mungu.


Heri taifa ambalo limejaliwa hayo! Heri taifa ambalo Yawe ndiye Mungu wao!


Na Yesu akamwambia: “Umeamini kwa sababu umeniona? Heri wale wanaoamini pasipo kuona!”


“Enyi wajinga! Mpaka wakati gani mutapenda kuwa wajinga? Mpaka wakati gani wenye kuzarau watafurahia mazarau yao, na wapumbafu kuchukia maarifa?


Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu.


Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.


Yawe anawalinda wageni, anawasaidia wajane na wayatima; lakini anaharibu mipango ya waovu.


Heri mutu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mutu anayemutumainia Yawe, Mungu wake,


Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.


Heri yenu ninyi Waisraeli. Nani anayekuwa kama ninyi, watu muliookolewa na Yawe, ambaye ndiye ngao ya musaada wenu, na upanga unaowaletea ushindi! Waadui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu, nanyi mutawakanyaga chini.”


Niliwaonya wazao wao kule katika jangwa: Musifuate masharti ya wazee wenu, musishike maagizo yao wala musijichafue kwa kuziabudu sanamu za miungu yao.


Azabu iko tayari kwa wenye kuzarau, na mapigo kwa migongo ya wapumbafu.


Ee Mungu, usikilize malalamiko yangu. Uyalinde maisha yangu kutoka vitisho vya waadui.


Mungu anipime katika mizani ya haki, naye ataona kwamba sina kosa. Kama nimeishi kwa kufuata uongo, kama nimekimbilia kudanganya watu,


Ni sawa kwako kunionea, kuzarau kazi ya mikono yako na kupendelea mipango ya waovu?


Alikuwa akishirikiana na Mungu, akatoweka, kwa maana Mungu alimupeleka.


Kwa sababu mama yake alikuwa mushauri wake katika kutenda maovu, naye vilevile alifuata mienendo ya jamaa ya Ahabu.


Halafu Yesu akamwambia: “Heri kwako, wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana hakuna mutu aliyekufunulia neno hili isipokuwa Baba yangu anayekuwa mbinguni.


na kila nyama mwenye kwato zinazogawanyika sehemu mbili na mwenye kucheua.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite