Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yuda 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Atakuja kuwahukumu wote na kuwaazibu watu wabaya wasiomwogopa Mungu, kwa ajili ya matendo yao yote mabaya waliyotenda, na kwa ajili ya maneno yote mabaya wenye zambi hawa waliyosema juu yake.”

Gade chapit la Kopi




Yuda 1:15
35 Referans Kwoze  

Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Hiyo ndiyo itakayotokea siku ile Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya watu kwa njia ya Yesu Kristo, kama vile Habari Njema yangu inavyosema.


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Vilevile ni sherti kujua kwamba Sheria haikuwekwa kwa ajili ya wenye haki, lakini kwa ajili ya watenda mabaya, waasi, watu wasiomuheshimu Mungu, wenye zambi, nao wenye kuchafua vitu vitakatifu na kukufuru, na kwa ajili ya wale wanaowaua wababa zao au wamama zao, na wauaji wowote.


Lakini wewe, kwa sababu gani unamuhukumu ndugu yako? Au wewe kwa sababu gani unamuzarau ndugu yako? Maana sisi wote tutasimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Mungu.


Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.


Kwa maana amekwisha kupanga siku atakapohukumu dunia kwa haki, kwa njia ya mutu mumoja, yule aliyemuweka kwa kazi ile. Naye amehakikisha mambo hayo kwa kumufufua mutu yule.”


Vilevile amemupa Mwana mamlaka ya kuhukumu, kwa sababu yeye ni Mwana wa Mutu.


Mushangilie mbele ya Yawe, maana anakuja kutawala dunia. Atahukumu ulimwengu kwa haki, atatawala mataifa kama vile inavyofaa.


Muache kujisifu, muache kusema kwa kiburi. Maana anayejua ni Yawe. Yeye anayapima matendo yote.


Tena Musa akasema: “Magaribi, Yawe atawapa nyama mupate kula na asubui atawapa mikate mupate kula na kushiba. Maana yeye ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie? Musitunungunikie sisi lakini mumunungunikie Yawe.”


Mwenye kushuhudia maneno hayo anasema: “Ndiyo, ninakuja upesi!” Amina! Kuja Ee Bwana Yesu!


Kisha nikaona nyama wa pili wa ajabu akitokea ndani ya udongo. Alikuwa na pembe mbili zinazokuwa kama za mwana-kondoo naye alikuwa akisema kama nyoka mukubwa.


Watu hawa wanaendelea kunungunika na kuteta wengine. Wanaishi kufuatana na tamaa zao mbaya. Wanasema maneno ya majivuno na kujipendekeza kwa watu kusudi wapate faida toka kwao.


Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.


Vilevile nilitaka nielezwe juu ya zile pembe kumi alizokuwa nazo juu ya kichwa chake, na ile pembe moja iliyoota na pembe zingine tatu zilizoanguka mbele yake, ndiyo ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa ambacho kilisema maneno ya kujivuna, na ambayo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine.


Maana, Mungu atahukumu matendo yote, hata yale yanayotendwa kwa siri, yakuwe mazuri au mabaya.


kusudi wawaazibu sawa ilivyoamuriwa! Na huu ndio utukufu wa waaminifu wa Mungu. Haleluia!


Mpaka wakati gani waovu watajigamba kwa maneno? Watajivuna na kujitapa mpaka wakati gani?


Kwa vinywa vyao wanatukana mbingu; kwa ndimi zao wanajitapa katika dunia.


Ataifanya haki yako iangae kama mwangaza wa jua muchana kati.


Usiniache nifezeheke, ee Yawe, maana mimi ninakulilia; lakini uwaache waovu wafezeheke, uwaache wapotelee huko kuzimu.


Wanasema vibaya juu yako; wanasema maovu juu ya jina lako!


Nimesikia jinsi unavyojivuna na kusema maneno mengi juu yangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite