Yoshua 9:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Basi, wakamwendea Yoshua katika kambi kule Gilgali, wakamwambia yeye na Waisraeli: “Sisi tumetoka katika inchi ya mbali. Tafazali tunaomba mufanye agano nasi.”
Halafu nabii Isaya akamwendea mufalme Hezekia na kumwuliza: “Watu hawa wamesema nini? Na, wamekujia kutoka wapi?” Naye Hezekia akamujibu: “Wamenifikia kutoka inchi ya mbali.”
Wakamujibu: “Sisi, watumishi wako, tumetoka inchi ya mbali na tumekuja kwa maana tumesikia sifa za jina la Yawe, Mungu wenu. Tulipata habari za utukufu wake na yote aliyoyafanya katika inchi ya Misri.
Wagibeoni wakapeleka ujumbe kwa Yoshua kule katika kambi Gilgali, wakamwambia: “Tafazali, usitutupilie sisi watumishi wako. Ukuje mbio utusaidie na kutuokoa kwa maana wafalme wote wa Waamori kutoka inchi ya milima wamekuja kutushambulia.”