Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 8:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Nao wataendelea kutufuatilia mpaka wakuwe mbali na muji wao, maana watafikiri kwamba wanatukimbiza kama vile walivyofanya mbele. Sisi tutawaacha watufukuze.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 8:6
7 Referans Kwoze  

Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.


Kwa vile uovu hauazibiwi haraka, mioyo ya wanadamu inakusudia kutenda mabaya.


Watu wa Benjamina wakafikiri: “Tumewapiga kama nyakati zilizopita.” Lakini Waisraeli wakasema: “Sisi tukimbie kusudi tuwavute mbali na muji mpaka kwenye njia kubwa.”


Adui akajisemesha: ‘Nitawafuata na kuwakamata; nitagawanya vitu mpaka hamu yangu iishe. Tutafuta upanga wetu, tutawaangamiza kwa mukono wetu.’


Maana, mufalme wa Misri atafikiri: ‘Hao Waisraeli wanatangatanga, nalo jangwa limewazuia wasiweze kutoka.’


Mimi, pamoja na watu wote wanaokuwa pamoja nami, tutaukaribia muji. Watakapotoka inje kuja kutushambulia kama pale mbele, sisi tutawakimbia.


Hapo, ninyi mutatokea kutoka kule mulikokuwa munavizia na kuuteka muji, maana Yawe, Mungu wenu, atautia muji huo katika mikono yenu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite