Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 8:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Waisraeli wote pamoja na viongozi wao, wazee na waamuzi na wageni wote waliokuwa kati yao, wakasimama kila upande kuelekeana na Sanduku la Agano mbele ya makuhani Walawi waliokuwa wamelibeba Sanduku la Agano la Yawe. Nusu yao wakasimama mbele ya mulima Gerizimu na nusu nyingine wakasimama mbele ya mulima Ebali, kama vile Musa, mutumishi wa Yawe alivyoagiza pale mbele juu ya kubarikiwa kwa Waisraeli.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 8:33
22 Referans Kwoze  

Yawe atakapowafikisha kwenye inchi munayokwenda kurizi, mutatangaza baraka kutoka kwenye mulima Gerizimu, na laana kutoka kwenye mulima Ebali.


Mutakusanya wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, kusudi kila mumoja asikie maneno haya ya kujifunza kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kuwa waangalifu kushika maneno ya sheria hii.


Basi, Musa akaandika sheria hiyo, akawapa makuhani wa ukoo wa Lawi ambao walikuwa wakibeba Sanduku la Agano la Yawe, na wazee wote wa Israeli.


Kisha Yoshua akayakusanya makabila yote ya Waisraeli kule Sekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na wakubwa wa Waisraeli, nao wakakuja mbele ya Mungu.


Hao makuhani waliokuwa wanabeba lile Sanduku la Agano la Yawe walipotoka katikati ya muto Yordani, na kukanyaga ukingo wa muto, maji ya muto Yordani yakaanza kutiririka tena, na kufurika kama mbele.


wakawaambia watu: “Mutakapoliona Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, limebebwa na makuhani Walawi, mutaondoka na kulifuata;


akawaambia Walawi waliokuwa wanabeba lile Sanduku la Agano la Yawe:


Mutafuata sheria moja kila mutu atakayekosa bila kukusudia, akuwe ni mwanainchi Mwisraeli au ni mugeni anayeishi pamoja nanyi.


Ninyi na yeye mutakuwa chini ya sheria ileile moja na maagizo yaleyale.


Sheria zilezile zitaelekea Mwisraeli aliyezaliwa katika inchi na wageni watakaoishi kati yenu.”


Yoshua aliwaita Waisraeli wote pamoja na viongozi na wazee wao, waamuzi na wakubwa, akawaambia: “Sasa mimi nimekuwa muzee wa miaka mingi.


Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawaita makuhani, akawaambia: “Mulibebe Sanduku la Agano na makuhani saba watwae mabaragumu saba ya kondoo dume, watangulie mbele ya Sanduku la Yawe.”


Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano, walisimama katikati ya muto Yordani mpaka watu walipomaliza kutimiza kila kitu ambacho Yawe alimwamuru Yoshua awaambie watu; Yoshua alifanya yote ambayo Musa alikuwa amemwamuru. Watu wakaharakisha kuvuka muto,


Basi, watu waliondoka katika kambi zao kwa kwenda kuvuka muto Yordani, nao makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano walitangulia watu.


Sheria hii inaelekea mugeni na mwenyeji. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Kisha akawaambia makuhani: “Mutwae Sanduku la Agano, mutangulie nalo mbele ya watu.” Nao wakalitwaa na kutangulia mbele ya watu.


Babu zetu walimwabudu Mungu juu ya mulima huu, lakini ninyi Wayuda munasema kama Yerusalema ni pahali pa kumwabudia Mungu.”


Katika vizazi vyote vinavyokuja, masharti yaleyale mutakayofuata ninyi ndiyo mugeni yeyote atakayeishi pamoja nanyi atakayofuata; mbele ya Yawe mutakuwa sawa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite