Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 7:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Halafu wakalundika mawe mengi juu yake, ambayo yako mpaka leo. Hapo hasira ya Yawe ikapoa; na pahali pale pakaitwa Bonde la Akori, ni kusema Bonde la Taabu, mpaka hivi leo.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 7:26
22 Referans Kwoze  

Nitamulipiza kwa ajili ya siku alizoabudu sanamu za mungu Bali, kwa ajili ya muda alioutumia kuzifukizia ubani, akajipamba kwa pete zake na ushanga, na kuwaendea wapenzi wake, akanisahau mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Bonde la Saroni litakuwa nafasi ya kukulishia nyama, bonde la Akori litakuwa mapumziko ya ngombe kwa ajili ya watu wangu walionitafuta.


Mutakusanya vitu vyote mulivyoteka katika kiwanja cha muji na kuchoma kwa moto vitu vile vyote kama vile sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yawe, Mungu wenu. Muji huo utakuwa lundo la mabomoko milele, nao hautajengwa tena.


Walinitupa ndani ya shimo nikiwa muzima na juu yangu wakalundika mawe.


Wakamukamata Abusaloma, wakamutupia ndani ya shimo kubwa katika pori na kulundika lundo kubwa sana la mawe juu yake. Watu wote wa Israeli wakakimbia, kila mumoja kwake.


Kisha akamutundika mufalme wa Ai juu ya muti wa tini mpaka magaribi. Lakini jua lilipoanza kutua, Yoshua aliamuru maiti yake iondolewe juu ya muti na kutupwa kwenye mulango wa muji kisha walundike lundo kubwa la mawe juu ya maiti hiyo. Lundo hilo liko kule mpaka leo.


Yoshua pamoja na Waisraeli wote, wakamukamata Akana mwana wa Zera, pamoja na feza, nguo, zahabu, watoto wake wa kiume na wabinti zake, ngombe, punda na kondoo wake, hema lake na kila kitu alichokuwa nacho na kuwapeleka kwenye bonde la Akori.


Kisha yule malaika aliyeongea nami akaniambia kwa sauti: Wale farasi waliokwenda katika inchi ya kaskazini wameituliza kasirani ya Yawe.


Yawe anaipenda inchi yake anawahurumia watu wake.


Munapasua nguo zenu kwa kuonyesha huzuni, lakini inafaa mioyo yenu ipasuke vilevile. Murudilie Yawe, Mungu wenu. Yeye amejaa huruma na rehema, hakasiriki upesi, ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia zake kusudi asiazibu.


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Basi, watu wa Daudi wakaizika mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani katika inchi ya Benjamina, kule Zela katika kaburi la Kisi baba ya Saulo. Walifanya kila kitu ambacho mufalme aliamuru. Nyuma ya hayo, Yawe akayakubali maombi kwa ajili ya inchi.


Wakati jua lilipokuwa karibu kutua, Yoshua aliamuru waondolewe juu ya miti walipokuwa wametundikwa na kutupwa katika pango walimokuwa wamejificha. Kisha wakaweka mawe makubwa kwenye mulango wa pango, nayo mawe hayo yako kule mpaka leo.


Ukifanya hivyo, hakika Wamisri watasema: Aliwatoa kwa nia mbaya kwa kuwaua kwenye mulima na kuwateketeza kabisa katika dunia. Ee Yawe, tuliza hasira yako kali na kuacha jambo hilo baya ulilokusudia kufanya juu ya watu wako.


na kumufuatilia yule Mwisraeli mpaka ndani ya hema, akawachoma mukuki wote wawili ndani ya tumbo. Ugonjwa mukali uliokuwa umewaangamiza Waisraeli ukakomeshwa.


Kitu ambacho kimekwisha kutolewa kiteketezwe musikitwae, kusudi Yawe aache ile hasira yake mbaya. Yawe, Mungu wenu, atawaonyesha rehema na kuwafanya ninyi mukuwe wengi sana kama vile alivyoahidia babu zenu,


Sasa, nimeamua ndani ya moyo wangu kufanya agano na Yawe, Mungu wa Israeli, kusudi asitukasirikie zaidi.


Afazali wakubwa wetu wabaki Yerusalema kushugulikia jambo hili kwa ajili ya watu wote. Kisha, kila mumoja ambaye ameoa mwanamuke wa kigeni akuje kwa zamu pamoja na viongozi na waamuzi wa muji wake, mpaka pale kasirani kali ya Mungu wetu itakapoondolewa kwetu.”


Umezuia kasirani yako yote; umeacha hasira yako kali.


Huko nitamurudishia mashamba yake ya mizabibu. Bonde la Akori litakuwa mulango wa tumaini. Ataniitikia vizuri kama vile alipokuwa kijana, kama wakati alipotoka katika inchi ya Misri.


Basi, wakamukamata Yona, wakamutupa ndani ya bahari na palepale bahari ikatulia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite