Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 7:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Yoshua akamwambia Akana: “Mwana wangu, umutukuze Yawe, Mungu wa Israeli, umusifu na kisha uniambie yale uliyotenda, wala usinifiche.”

Gade chapit la Kopi




Yoshua 7:19
25 Referans Kwoze  

Basi mufanye sanamu zenu za majipu na sanamu za panya, vitu ambavyo vinaangamiza inchi yenu, nanyi mutamutukuza Mungu wa Israeli. Labda ataacha kuwaazibu ninyi wenyewe, miungu yenu na inchi yenu.


Mumutukuze Yawe, Mungu wenu, mbele hajawaletea giza, mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza. Ninyi mulitazamia mwangaza, lakini anaugeuza kuwa usiku anaufanya kuwa giza nzito.


Halafu wakubwa wa Wayuda wakamwita yule aliyekuwa kipofu kwa mara ya pili na kumwambia: “Sema ukweli mbele ya Mungu! Kwa ngambo yetu tunajua kwamba mutu yule ni mwenye zambi.”


Nilimwomba Yawe, Mungu wangu, na kuitikia zambi, nikisema: Ee Bwana, wewe ni Mungu mukubwa na wa kuogopesha. Wewe unashika agano lako na kutenda mema kwa wanaokupenda na kuzitii amri zako.


Mufalme Hezekia aliwasifu na kuwatia moyo makuhani kwa sababu waliendesha ibada kwa ujuzi mwingi. Nyuma ya kumaliza siku saba ambamo watu walikula, wakatoa sadaka za amani na kumutukuza Yawe, Mungu wa babu zao,


Kwa hiyo Saulo akamwambia Yonatani: “Uniambie jambo ulilofanya.” Yonatani akajibu: “Nilikula asali kidogo kwa kutumia fimbo yangu. Niko hapa na niko tayari kufa.”


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Kisha niliitikia makosa yangu mbele yako, wala sikuficha uovu wangu. Nilisema kwamba nitaungama makosa yangu mbele ya Yawe. Nawe ukanisamehe zambi yangu.


Watu wakaunguzwa na lile joto kali, hata wakatukana jina la Mungu anayekuwa na uwezo wa kuamuru mapigo yale. Wakakataa kugeuka toka zambi zao na kumutukuza Mungu.


Kwa maana mutu mwenye kasirani hawezi kutimiza mambo ya haki mbele ya Mungu.


Uwaambie wazee wanaume wakuwe wakadirifu, wenye heshima na utaratibu, wenye kukamilika katika imani, katika upendo na uvumilivu.


Anapaswa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye; kwa maana labda Mungu anaweza kuwajalia hata wapate kugeuka toka zambi na kutambua ukweli.


Kwa maana mutu akiamini kwa moyo wake, Mungu anamuhesabia haki mbele yake; naye anapoitikia kwa kinywa chake, anaokolewa.


Hakuna mwingine kati yao aliyerudia kwa kumutolea Mungu shukrani, isipokuwa huyu mugeni tu?”


Nitawafanya watu kuwa wachache kuliko zahabu safi; wanadamu watakuwa wachache kuliko zahabu ya Ofiri.


Unihurumie, ee Mungu, kadiri ya wema wako; uyafute makosa yangu, kadiri ya wingi wa rehema yako.


Akana akamujibu: “Ni kweli nimetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wa Israeli. Na hivi ndivyo nilivyofanya:


Halafu akamwuliza: “Wameona nini katika nyumba yako?” Hezekia akamujibu: “Wameona yote yanayokuwa katika nyumba yangu. Hakuna kitu chochote katika akiba zangu ambacho sikuwaonyesha.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite