Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 5:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kisha Yawe akamwambia Yoshua: “Leo hii nimewaondolea ile haya ya Misri.” Hivyo pahali pale pakaitwa Gilgali mpaka hivi leo.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 5:9
21 Referans Kwoze  

Daudi akawauliza wale waliokuwa karibu naye: “Mutu atakayemwua Mufilistini huyu na kuikomboa Israeli kutokana na haya hii atafanyiwa nini? Ni nani huyu Mufilistini, mutu mupagani, anayesubutu kuwatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima?”


Waisraeli walivuka muto Yordani katika siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, wakapiga kambi kule katika muji wa Gilgali, upande wa mashariki wa Yeriko.


Wakawaambia: “Hatuwezi kumwoesha dada yetu kwa mutu asiyetahiriwa. Kufanya hivyo ni haya kwetu.


Umuondoe kijana aliyetukana inje ya kambi, wale wote waliomusikia akitukana waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na wote pamoja wamwue kwa kumupiga mawe.


Aliendelea na uzinzi wake aliouanza kule Misri wakati huo wa ujana wake, wanaume walivunja ubikira wake na kuzitimiza tamaa zao kwake.


Katika ujana wao walipokuwa wanakaa kule Misri, wakakubali maziba yao kupapaswa, wakapoteza ubikira wao, wakafanya uzinzi.


Wamisri, Wayuda, Waedomu, Waamoni, Wamoabu na wakaaji wote wa jangwa wanaonyoa nywele zote za pembenipembeni ya kichwa. Maana watu hawa wote na Waisraeli wote hawajatahiriwa mioyo yao.


Uniepushe na matusi ninayoogopa; maana maamuzi yako ni mema.


Mimi mutumishi wako nimekwisha kuua simba wengi na dubu wengi. Sasa, hata yule Mufilistini mupagani, ambaye amewatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima, atakuwa kama wao.


Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”


“Sasa, basi, mumutii Yawe na kumutumikia kwa moyo wa haki na uaminifu. Muache kabisa miungu ile ambayo wazee wenu waliiabudu ngambo ya muto Furati na katika inchi ya Misri. Mumutumikie Yawe.


Wanaume wote walipokwisha kutahiriwa walikaa katika kambi mpaka walipopona.


Kila mwaka Samweli alitembelea Beteli, Gilgali na Misipa, na kuwaamulia Waisraeli haki zao katika miji hiyo yote.


Kwa hiyo, Daudi aliivuta mioyo ya watu wote wa Yuda kama mutu mumoja. Halafu, wakamupelekea ujumbe kusema: “Rudi kwako, wewe na watumishi wako wote.”


Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!


Nimeyasikia matusi ya Wamoabu na mazarau ya Waamoni, jinsi walivyowatusi watu wangu na kujivuna kwamba wamenyanganya inchi yao.


vilevile kutoka Beti-Gilgali, eneo la Geba na Azimaweti, kwa sababu waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kandokando ya Yerusalema.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Lakini musinitafutie kule Beteli wala musiende Gilgali wala musivuke kwenda Beri-Seba. Maana wakaaji wa Gilgali, hakika watapelekwa katika uhamisho, na Beteli utaangamizwa!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite