Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 4:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yoshua akasimika vilevile mawe kumi na mawili katikati ya muto Yordani, pahali pale miguu ya makuhani waliobeba lile Sanduku la Agano iliposimama. Mawe hayo yako kule mpaka hivi leo.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 4:9
16 Referans Kwoze  

Kisha, Samweli alitwaa jiwe na kulisimamisha kati ya Misipa na Seni, akaliita jiwe hilo “jiwe la musaada”, akisema: “Yawe ametusaidia mpaka sasa.”


Kwa sababu miti ile ilikuwa mirefu sana, incha zake ziliweza kuonekana kutoka Pahali Patakatifu mbele ya chumba cha ndani, lakini haikuweza kuonekana kutoka upande wa inje. Miti ile ingali pahali pale hata leo.


Wakaaji wa Beroti walikimbilia Gitaimu, na wameishi kule kama wageni mpaka leo.


Tangu siku ile Daudi alifanya uamuzi ule kuwa sharti na agizo katika inchi ya Israeli mpaka hivi leo.


Mutu yule akahamia katika inchi ya Wahiti, kule akajenga muji ambao aliuita Luzi, na muji huo unaitwa hivyo mpaka leo.


Yoshua akayaandika haya yote katika kitabu cha sheria ya Mungu; kisha, akatwaa jiwe kubwa na kulisimika chini ya muti wa mwalo katika hema ya Yawe.


Alizikwa katika bonde la Moabu, kuelekea muji wa Beti-Peori; lakini mpaka leo, hakuna mutu anayejua pahali alipozikwa.


Basi, kutakuwa mawe kumi na mawili yaliyochorwa majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Kila moja litakuwa kama muhuri, kwa kusimamia makabila yale kumi na mawili.


Yawe akamwambia Musa: Kuja kwangu juu kwenye mulima, ungoje kule. Mimi nitakupa vibao vya mawe vyenye sheria na amri nilizoandika kwa ajili ya kuwafundisha Waisraeli.


Yakobo akaamuka asubui mapema, akatwaa lile jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake, akalisimika kama nguzo na kulitakasa kwa kulimiminia mafuta.


Basi, Isaka akakiita kisima hicho Siba, ni kusema “Kiapo”. Kwa hiyo jina la muji ule ni Beri-Seba hata leo.


Basi wale waaskari walinzi wakapokea zile feza na kufanya sawa walivyoambiwa. Na habari hii ilienea katikati ya Wayuda mpaka leo.


Ni kutokana na mambo hayo yote shamba lile linaitwa “Shamba la Damu” hata leo.


Alitwaa mawe kumi na mawili, hesabu ya makabila kumi na mawili yaliyopewa majina ya wana wa Yakobo ambaye neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Jina lako litakuwa Israeli.”


Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano, walisimama katikati ya muto Yordani mpaka watu walipomaliza kutimiza kila kitu ambacho Yawe alimwamuru Yoshua awaambie watu; Yoshua alifanya yote ambayo Musa alikuwa amemwamuru. Watu wakaharakisha kuvuka muto,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite