Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 4:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Mutawaambia kwamba Yawe, Mungu wenu, aliyakausha maji ya muto Yordani kwa ajili yenu mpaka mukavuka, kama vile alivyofanya kwa bahari Nyekundu. Akaikausha mbele yetu mpaka tulipovuka

Gade chapit la Kopi




Yoshua 4:23
8 Referans Kwoze  

Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari, naye Yawe akasukuma bahari nyuma kwa upepo mukali toka upande wa mashariki. Upepo ule ulivuma usiku kucha, ukagawanya bahari sehemu mbili na katikati kukatokea inchi kavu.


Zamani Yawe alifanya barabara katika bahari na kuweka njia kati ya maji mengi. Alipiga kundi la waaskari lenye nguvu, kundi la magari na farasi wa vita, waaskari na mashujaa wa vita. Aliwaangusha chini hata hawawezi kusimama tena, Aliwakomesha na kuwazimisha kama utambi wa taa. Sasa Yawe anasema hivi:


Aligawanya bahari, akawapitisha ndani yake; aliyafanya maji yasimame kama ukuta.


Uligawanya bahari katikati mbele yao, nao wakapita katikati ya bahari, pahali pakavu. Lakini ukawatupa Wamisri waliowafuatilia kama jiwe zito ndani ya maji mengi.


usikilize kutokea kwako mbinguni. Umujalie yule mugeni yote atakayokulilia, kusudi watu wote katika ulimwengu wapate kujua jina lako na kukutii kama watu wako Waisraeli wanavyofanya, na wapate kufahamu kwamba nyumba hii ambayo nimeijenga, inajulikana kwa jina lako.


Wakati farasi wa mufalme wa Misri na magari yake pamoja na wapanda-farasi wake walipoingia pahali pakavu katika bahari, Yawe aliyarudisha maji ya bahari yakawafunika. Lakini Waisraeli waliendelea kutembea pakavu katikati ya bahari.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite