Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 24:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Mukimwacha Yawe na kuitumikia miungu ya kigeni, atawaazibu na kuwaangamiza ninyi, hata ingawa amewatendea mema haya yote.”

Gade chapit la Kopi




Yoshua 24:20
19 Referans Kwoze  

Basi Mungu akajitenga mbali nao, akawaacha waabudu nyota, jua na mwezi kufuatana na maneno haya yaliyoandikwa katika kitabu cha manabii: ‘Ninyi watu wa Israeli, si mimi muliyemuchinjia nyama na kumutolea sadaka zingine kwa muda wa ile miaka makumi ine katika jangwa.


Lakini, mutu wa haki akiacha haki yake na kutenda uovu na kufanya machukizo yaleyale mutu mwovu anayofanya, basi, huyo ataishi? Hapana! Matendo yake yote mema aliyotenda hayatakumbukwa tena; atakufa kwa sababu ya uasi na zambi aliyotenda.


Ee Yawe, tumaini la Waisraeli, wote wanaokukataa wafezeheshwe. Wanaokuacha wewe watatoweka, kama majina yaliyoandikwa chini katika mavumbi, kwa maana wamekuacha wewe Yawe, unayekuwa chemichemi ya maji ya uzima.


“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Lakini wao waliasi, wakaihuzunisha roho yake takatifu. Basi, Mungu akageuka, akakuwa adui yao; yeye mwenyewe akapigana nao.


Lakini waasi na wenye zambi wote wataangamizwa pamoja; wanaomwacha Yawe watateketezwa.


Ingekuwa haya kubwa kwangu kumwomba mufalme kundi la waaskari na waaskari wapanda-farasi wa kutulinda na waadui katika njia maana nilikuwa nimekwisha kumwambia kwamba Mungu wetu anawabariki wote wanaomutafuta, lakini anawachukia na kuwaazibu wote wanaomwacha.


naye akatoka kwenda kukutana na mufalme Asa, akamwambia: “Unisikilize, ee Asa na watu wote wa kabila la Yuda na la Benjamina! Yawe yuko pamoja nanyi, ikiwa mutakuwa pamoja naye. Mukimutafuta, mutamupata, lakini mukimwacha, naye atawaacha.


Mwenye haki mbele yangu ataishi kwa njia ya imani. Lakini kama akirudi nyuma, sitapendezwa naye.”


“Mimi leo ninaita mbingu na dunia zishuhudie juu yenu. Mutakapokuwa mukikaa katika inchi hiyo, mukipata watoto na wajukuu na kuwa wazee, kama mukianza kupotoka na kujifanyia sanamu katika umbo la kitu chochote, mukifanya uovu mbele ya Yawe, Mungu wenu, na kumukasirikisha, mara moja mutaangamia kabisa katika inchi ambayo munaenda kurizi huko ngambo ya muto Yordani. Hamutaishi huko muda murefu, lakini mutaangamizwa kabisa.


Nao watu wakamwambia Yoshua: “Hapana! Sisi tutamutumikia Yawe tu.”


Lakini kama hamutasikiliza sauti ya Yawe, mukiasi amri yake, basi yeye atapambana nanyi pamoja na mufalme wenu.


Lakini kama mukiendelea kutenda maovu, mutaangamia ninyi wenyewe pamoja na mufalme wenu.”


“Basi sasa, mbele ya kusanyiko hili la Waisraeli wote, taifa la watu wa Yawe, na mbele ya Mungu wetu, muangalie na mushike amri zote za Yawe, Mungu wenu, kusudi muendelee kurizi inchi hii nzuri, na kuwarizisha wazao wenu nyuma yenu, hata milele.


“Lakini wazao wake wakiiacha sheria yangu, wasipoishi kufuatana na maagizo yangu,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite