13 “Niliwapa mashamba ambayo hamukukuwa mumeyalima, na miji ambayo hamukuijenga ambamo sasa munaishi, na kula matunda ya mizabibu na mizeituni ambayo hamukuipanda.
Yawe, Mungu wenu, anawaleta kwenye inchi nzuri, inchi yenye vijito na chemichemi, na maji yanayobubujika kutoka bonde na milima;
Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.
Hakuna hata ahadi yoyote njema ambayo Yawe aliiahidi Waisraeli ambayo haikutimia. Ahadi zote zilitimia.
Lakini Waisraeli hawakuiteketeza miji iliyokuwa kwenye vilima, isipokuwa tu muji wa Hazori ambao Yoshua aliuteketeza.
Nami nitawapeleka katika inchi ile niliyoapa kumupa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Nitawapa inchi hiyo ikuwe yenu. Mimi ni Yawe.’ ”
“Wakati Yawe, Mungu wenu, atakapoteketeza watu wale ambao anawapa ninyi inchi yao, na kisha kuitwaa na kuishi katika nyumba zao,