Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 23:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Musishirikiane na mataifa haya yaliyobaki kati yenu. Musiitaje miungu yao wala musiape kwa majina ya miungu yao; musiitumikie wala kuinama mbele yao.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 23:7
23 Referans Kwoze  

Ushike mambo yote niliyokuambia. Usiyataje hata kidogo majina ya miungu mingine, hayo yasisikilike katika kinywa chako.


Yawe anauliza: Namna gani nitaweza kukusamehe, ee Yerusalema? Watu wako wameniasi; wameapa kwa majina ya miungu ya uongo. Nilipowashibisha kwa chakula, wao walifanya uzinzi, wakakusanyika kwa uwingi katika nyumba za makahaba.


Lakini wanaoabudu miungu mingine, watapata mateso mengi. Sitaitolea sadaka za damu hata kidogo, na majina ya miungu hiyo sitayataja.


Musiwaruhusu waishi katika inchi yenu wasiwasukume kutenda zambi mbele yangu. Maana kama mukitumikia miungu yao, hakika ile itakuwa mutego wa kuwanasa.


Musishiriki katika matendo ya giza yasiyofaa, lakini muyafichue.


Musidanganyike: “Warafiki wabaya wanaharibu tabia nzuri za watu.”


Nitawaangamiza wote wanaoinama juu ya dari, wakiabudu jeshi la mbinguni. Nitawaangamiza wale wanaoniabudu na kuapa kwa jina langu, tena wanaapa vilevile kwa jina la mungu Milkomu.


Usijiingize katika njia ya waovu, wala usifuate mwenendo wa watu wabaya.


Maana, kama mukimwasi Yawe na kujiunga na mataifa haya yaliyobaki kati yenu, mukioa kwao nao wakioa kwenu,


Huko nitamurudishia mashamba yake ya mizabibu. Bonde la Akori litakuwa mulango wa tumaini. Ataniitikia vizuri kama vile alipokuwa kijana, kama wakati alipotoka katika inchi ya Misri.


Nebo na Bali-Meoni (majina ya hiyo miji yalibadilishwa), na Sibuma. Miji waliyoijenga wakaipa majina mengine.


Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.


Mutamwogopa Yawe, Mungu wenu, mutamutumikia yeye peke yake na kuapa katika jina lake peke yake.


Mumwogope Yawe, Mungu wenu, mumutumikie, muambatane naye na kuapa kwa jina lake.


Lakini muambatane na Yawe, Mungu wenu, kama mulivyofanya mpaka leo.


Na kama watajifunza mwenendo wa watu wangu kwa moyo wote, wakiapa kwa jina langu, wakisema “Kama vile Yawe anavyoishi”, kama vile walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la mungu Bali, basi watastawi katikati ya watu wangu.


Lakini kama musipowafukuza wenyeji wa inchi hiyo kwanza, basi wale mutakaowaacha watakuwa kama vile sindano ndani ya macho yenu au miiba kila upande, na watawasumbua.


Musiabudu miungu mingine, miungu ya watu wanaokuwa jirani nanyi,


Naye Yawe anisamehe ninapofuatana na mufalme wangu kwenda kuabudu katika hekalu la Rimoni mungu wa Waaramu. Ninapaswa kuinama pamoja naye kwa sababu anaegemea kwenye mukono wangu. Ninaomba Yawe anisamehe!”


na walitumikia sanamu ambazo Yawe alikuwa amewakataza, akisema: “Musifanye hivyo.”


“Lakini mukiacha kunifuata, na kuasi maongozi yangu na amri nilizowapa, na kwenda kutumikia miungu mingine na kuiabudu,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite