Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 23:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 “Sasa, wakati wangu wa kufa kama inavyokuwa kawaida ya wanadamu wote umekaribia. Lakini ninyi wote munajua wazi ndani ya mioyo na roho zenu kwamba katika mambo yote mema ambayo Yawe, Mungu wenu aliwaahidi, hakuna hata moja ambalo halikutimia. Yote yametimia kama vile alivyoahidi.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 23:14
16 Referans Kwoze  

Mbingu na dunia vitatoweka, lakini maneno yangu hayatabadilika hata kidogo.


“Mwana wangu, kama inavyokuwa kawaida kwa viumbe vyote kufa, siku zangu zimekwisha. Ukuwe imara na hodari.


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


“Atukuzwe Yawe ambaye amewapatia watu wake Waisraeli amani, kulingana na ahadi yake. Ametimiza ahadi zake zote njema alizozitoa kupitia kwa mutumishi wake Musa.


Samweli aliendelea kukomaa na Yawe akakuwa pamoja naye, na yale yote aliyosema hakuna hata moja ambalo halikutimia.


watu wanaogopa mupando na kutishwa katika njia, muti wa lozi unachanua maua yake meupe, mapanzi hayawezi kuruka, hakuna hamu tena, mwanadamu anaelekea kwenye makao yake ya milele, waombolezaji wanasambaa katika njia,


na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Kweli! Ninajua utanipeleka tu katika kifo, pahali wote wanaoishi watakapokutana.


Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.


Wakati wa kufa kwake ulipokaribia, Yakobo akamwita mwana wake Yosefu, akamwambia: “Sasa, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, weka mukono wako chini ya mapaja yangu, uniahidi kwamba utanitendea kwa wema na uaminifu. Usinizike huku Misri,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite