Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 23:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Mutu wenu mumoja tu anaweza kuwakimbiza waadui elfu moja, maana Yawe Mungu wenu ndiye anayewapigania kama alivyowaahidi.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 23:10
27 Referans Kwoze  

Mutu mumoja anaweza namna gani kuwashinda watu elfu moja, au watu wawili wanaweza namna gani kuwashinda watu elfu kumi, isipokuwa kama mulinzi wao amewatupa, Yawe amewaacha?


Watano wenu watafukuza waadui mia moja na mia moja wenu watafukuza waadui elfu kumi. Waadui zenu wataangamia mbele yenu kwa upanga.


Musiwaogope maana Yawe, Mungu wenu, ndiye atakayepigana kwa ajili yenu.’


Yawe atawapigania. Ninyi mutakaa kimya tu.”


Zaburi ya Daudi. Uwapinge, ee Yawe, hao wanaonipinga; uwashambulie hao wanaonishambulia.


maana Yawe, Mungu wenu, ndiye atakayekwenda pamoja nanyi kupigana kwa ajili yenu mbele ya waadui zenu na kuwapa ushindi’.


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika; Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.


Ninyi mumeona mambo yote Yawe, Mungu wenu, aliyoyatendea mataifa haya yote kwa ajili yenu. Yawe, Mungu wenu, ndiye aliyewapigania.


Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”


Aliweza kuitwaa inchi hii yote kwa sababu Yawe, Mungu wa Israeli, aliwapigania Waisraeli.


Samusoni akaona mufupa mubichi wa taya ya punda, akautumia kuwaua watu elfu moja.


Haya ni majina ya mashujaa Daudi aliokuwa nao: Yosebu-Basebeti, wa muji wa Takemoni ndiye aliyekuwa kiongozi wa wale watatu. Yeye alipigana kwa mukuki wake, akaua watu mia nane mara moja katika vita.


Nyuma ya Ehudu mwana wa Anati, Samugari akakamata nafasi yake. Yeye aliwaua Wafilistini mia sita kwa fimbo ya kuchunga ngombe. Naye vilevile aliwakomboa Waisraeli.


‘Watu wa Israeli musikilize! Leo munakaribia kupigana na waadui zenu. Musivunjike moyo, au kuogopa, au kutishwa, au kuwaogopa waadui;


Waadui zenu wakiwashambulia, Yawe atawapa ushindi juu yao. Wakikuja kuwashambulia kwa njia moja watawakimbia kwa njia saba.


Akasema hivi: Nitawaficha uso wangu nione mwisho wao utakuwa namna gani. Maana wao ni kizazi kipotovu, watoto wasiokuwa na uaminifu wowote.


Basi, mukuwe waangalifu sana kumupenda Yawe, Mungu wenu.


Wakaua waadui wengi sana kwa sababu vita hiyo ilikuwa ni vita ya Mungu. Nao waliendelea kuishi katika inchi ile, mpaka wakati wa uhamisho.


Watu wenu elfu moja watamukimbia askari mumoja adui; na waaskari watano waadui watawakimbiza ninyi wote. Kwa mwisho, watakaobaki, watakuwa kama muti wa bendera kwa mulima, kama kitambulisho kinachokuwa juu ya kilima.


Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.


Mutafukuza waadui zenu na kuwaua kwa upanga.


Waliweka tumaini lao kwa Mungu na wakamwomba awasaidie, naye akaitikia ombi lao na kuwatia katika mikono yao Wahagari pamoja na warafiki zao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite