Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 22:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Basi, Yoshua akawabariki na kuwaruhusu waende zao akawaambia:

Gade chapit la Kopi




Yoshua 22:6
18 Referans Kwoze  

Halafu Yoshua akamubariki Kalebu mwana wa Yefune na kumupa muji wa Hebroni kuwa sehemu yake.


Kisha Yesu akatoka nao katika muji na kwenda karibu na kijiji cha Betania na pale akainua mikono yake juu na kuwabariki.


Daudi alipomaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na za amani, aliwabariki watu kwa jina la Yawe wa majeshi,


Musa akachunguza kila kitu, akaona kwamba walikuwa wamefanya kila kitu kama vile Yawe alivyoamuru. Hivyo Musa akawabariki.


Kisha, Yosefu akamuleta baba yake Yakobo kumwamukia mufalme. Naye Yakobo akamupa mufalme baraka zake.


Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,


Watu wengi kati ya wale waliotoka katika kabila la Efuraimu, Manase, Isakari na Zebuluni, walikuwa wakifanya Pasaka kinyume cha maagizo. Hii ni kwa kuwa mufalme Hezekia aliwaombea akisema: “Yawe, wewe ni mwema. Umusamehe mutu yeyote


Daudi aliporudi kwake kwa kuibariki jamaa yake, Mikali, binti ya Saulo, alikwenda kumupokea, akasema: “Ni ajabu kwa mufalme wa Waisraeli kujiheshimu leo, kwa kujifunua uchi wake mbele ya watumishi wake na wajakazi wake sawa vile mushenzi anavyovua nguo zake mbele ya watu bila haya!”


Eli aliwabariki Elekana na muke wake, akisema: “Yawe akupe wewe Elekana watoto wengine kwa mwanamuke huyu kusudi wakamate nafasi ya yule uliyemupa Yawe.” Kisha wao walirudi kwao.


Kisha Yakobo akamubariki mufalme, akaondoka.


akamubariki Abramu akisema: “Abramu abarikiwe na Mungu Mukubwa, Muumba wa mbingu na dunia!


Halafu Yoshua akawaruhusu watu waondoke; nao wakaenda kila mumoja kwake.


Kisha, Samweli aliwaelezea watu juu ya mapaswa na haki za mufalme, akaziandika katika kitabu ambacho alikiweka mbele ya Yawe. Kisha, Samweli aliwaaga watu wote, kila mutu aende kwake.


Saulo aliwachagua Waisraeli elfu tatu. Kati yao, elfu mbili alikuwa nao kule Mikimasi na katika inchi ya milima ya Beteli. Elfu moja aliwaweka kule Gibea katika eneo la Benjamina. Hao aliwaweka chini ya uongozi wa mwana wake Yonatani. Watu wengine wote waliobakia, aliwarudisha, kila mutu kwake.


na akawagawanyia watu wote, kundi lote la Waisraeli, wanaume na wanawake, kila mumoja, mukate, kipande cha nyama na mukate wa sadaka. Kisha, watu wote waliondoka, kila mutu akarudi kwake.


Katika siku ya nane, Solomono aliwaaga watu; nao wakamutakia mufalme baraka, wakaenda kwao wakishangilia na kufurahi kwa sababu ya wema ambao Yawe aliuonyesha kwa Daudi, mutumishi wake, na kwa watu wake Waisraeli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite