Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 22:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Sasa Yawe, Mungu wenu, amewapa wandugu zenu amani, kama vile alivyoahidi, basi, murudie kwenu katika inchi ambayo mulipewa na Musa mutumishi wa Yawe, ikuwe mali yenu, ni kusema ngambo ya muto Yordani.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 22:4
16 Referans Kwoze  

Makabila ya Rubeni, Gadi na nusu nyingine ya kabila la Manase yalikuwa yamepewa inchi inayokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa, mutumishi wake.


Hatutarudi kwenye nyumba mpaka pale Waisraeli wengine wote watakaporizi maeneo yao waliyogawanyiwa.


Muwasaidie wandugu zenu Waisraeli mpaka Yawe atakapowajalia watulie pahali pao kama vile nanyi mulivyotulia, ni kusema nao vilevile warizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapatia huko ngambo ya Yordani. Nyuma ya hayo, mutaweza kurudia katika inchi yenu hii ambayo nimewapa ikuwe yenu!’


Sehemu ya inchi ambayo Musa aliwapa watu wa kabila la Rubeni kulingana na jamaa zao,


Kwa hiyo mukuwe waangalifu kushika maneno yote ya agano hili kusudi mupate kufanikiwa katika kazi zenu zote.


kwa sababu bado hamujaingia pahali pa kupumzikia na katika urizi Yawe, Mungu wenu, anaowapa.


Kwa maana kama Yoshua angekuwa amewafikisha watu kwenye mapumziko, Mungu hangesema tena nyuma ya pale juu ya siku ingine.


Mungu akasema: Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe na nitakupa raha.


Mutawasaidia mpaka Yawe atakapowapa wandugu zenu vilevile pahali pa kupumzika, kama vile alivyowapa ninyi, nao vilevile warizi inchi ambayo wanapewa na Yawe, Mungu wenu. Kisha mutarudi katika inchi ambayo ni mali yenu na kuirizi, inchi ambayo mulipewa na Musa, mutumishi wa Yawe, ngambo ya muto Yordani.”


Wala hamukuwaacha wandugu zenu kwa muda ule wote murefu mpaka leo, lakini mumefuata kwa uangalifu amri ya Yawe, Mungu wenu.


Musa mutumishi wa Yawe pamoja na Waisraeli aliwashinda wafalme hao, akawapatia inchi hizo makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase zikuwe mali yao kabisa.


“Yawe, Mungu wenu hayuko pamoja nanyi? Hajawapa amani katika pande zote? Yeye aliwatia wakaaji wa inchi hii katika mikono yangu na sasa wako chini ya Yawe na watu wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite