2 wakawaambia: “Yawe alimwagiza Musa kwamba tupewe miji ya kuishi na mbuga za malisho ya nyama wetu.”
Nyuma ya kuishinda ile inchi, Waisraeli wote pamoja wakakusanyika kule Shilo na kulisimika hema la kusanyiko.
Mwenye kufundishwa Habari Njema anapaswa kushirikiana mapato yake na yule anayemufundisha.
Vilevile musibebe mifuko, kanzu mbili, viatu wala fimbo, kwa sababu mutumishi anastahili kupewa posho lake.
Hata hivyo, nyumba zinazokuwa katika miji Walawi wanayorizi zinaweza kukombolewa wakati wowote.
Basi, Waisraeli wakaigawanya inchi kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Basi, kulingana na amri ya Yawe, Waisraeli walichagua kutoka katika maeneo ya inchi zao, miji na vijiji vya malisho, wakawapa Walawi ikuwe sehemu yao.