Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mufalme wa muji wa Yeriko akaambiwa: “Wanaume wawili Waisraeli wameingia katika muji leo usiku kwa kuipeleleza inchi.”

Gade chapit la Kopi




Yoshua 2:2
7 Referans Kwoze  

Mimi ni Mungu na nitakuwa Mungu siku zote. Hakuna anayeweza kuepuka nguvu yangu; hakuna anayeweza kupinga ninayofanya.


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Wimbo wa safari za kidini: wa Solomono. Yawe asipoijenga nyumba, wanaoijenga wanajisumbua bure. Yawe asipoulinda muji, wanaoulinda wanakesha bure.


Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kwa siri kutoka Sitimu waende kufanya upelelezi katika inchi ile na hasa muji wa Yeriko. Wakaenda, wakafika kwenye nyumba ya kahaba mumoja aliyeitwa Rahabu wakalala humo.


Mufalme wa Yeriko akatuma watu kwa Rahabu, akisema: “Uwatoshe inje watu waliokuja katika nyumba yako maana wamekuja kuipeleleza inchi yote.”


Kwa hiyo watu wa kabila la Dani wakachagua kati yao watu hodari, wakawatuma kutoka kule Estaoli na Zora, wakawaamuru waende kuipeleleza inchi. Basi watu hao wakafika katika inchi ya milima ya Efuraimu katika nyumba ya Mika, wakaenda na kukaa mule.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite