Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 2:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Tutakapokuja katika inchi hii, funga kamba hii nyekundu kwenye dirisha ambalo umetuteremushia. Uwakusanye hapa kwako baba yako, mama yako na kaka zako na jamaa yote ya baba yako.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 2:18
19 Referans Kwoze  

Basi, wale vijana wapelelezi wakaenda; wakamuleta Rahabu, baba yake na mama yake, wandugu zake na watu wote wa jamaa yake, wakawaweka inje ya kambi ya Israeli.


Naye akawaambia: “Ikuwe jinsi mulivyosema.” Kisha akawaruhusu waende zao, nao wakaondoka. Naye akaifunga ile kamba nyekundu kwenye dirisha.


Kwa maana, kwanza Musa aliwatangazia watu wote amri zote za Sheria. Kisha akatwaa damu ya ngombe pamoja na maji, naye akavinyunyiza juu ya kitabu cha Sheria na juu ya watu wote akitumia manyoya mekundu na vitawi vya muti wa hisopo.


Na pale pale nikatuma watu kwako, nawe umefanya vizuri kwa kufika. Sasa sisi wote tuko hapa mbele ya Mungu kwa kusikiliza mambo yote Bwana aliyokuagiza kutuambia.”


basi, kuhani ataamuru watu walete ndege wawili safi wanaokuwa wazima, kipande cha muti wa mwerezi, sufu ya rangi nyekundu na tawi la hisopo kwa ajili ya yule mutu atakayetakaswa.


Bwana awajalie mema sana watu wa jamaa ya Onesiforo, kwa maana amekuja mara nyingi kunifariji, wala hakusikia haya kwa kuniona niko katika kifungo.


Ni yeye atakayekuambia mambo yanayokupasa wewe pamoja na watu wote wa nyumba yako kusudi mupate kuokolewa.’


Petro akaingia ndani ya nyumba akiwa akisimulia na Kornelio, na mule akakuta watu wengi wamekusanyika.


Yesu akamwambia: “Leo nyumba hii imeokolewa, kwa sababu mutu huyu vilevile ni wa uzao wa Abrahamu.


Halafu kuhani atatwaa muti wa mwerezi, hisopo na sufu nyekundu na kuvitia katika moto huo.


Kisha, watavifunika vyombo hivi vyote kwa kitambaa chekundu, na juu yake wataweka kifuniko cha ngozi laini ya mbuzi. Halafu wataingiza miti yake ya kulibebea.


Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Yawe akamwambia Noa: “Ingia ndani ya chombo wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wa kizazi hiki, nimekuona wewe peke yako kuwa mutu wa haki mbele yangu.


Maana, ninaweza namna gani kuvumilia kuona watu wangu wanaangamizwa na wandugu zangu wanauawa?”


Midomo yako ni kama utepe mwekundu, kinywa chako kinapendeza kweli. Mashavu yako ni kama nusu mbili za makomamanga ndani ya ushungi wako.


Basi, ile damu itakuwa kitambulisho chenu cha kuonyesha nyumba mutakamokuwa. Nami nitakapoiona ile damu, nitawapita ninyi, hamutapatwa na hasara yoyote wakati nitakapoipiga inchi ya Misri.


Lakini yule kahaba Rahabu pamoja na watu wote wa nyumba ya baba yake, Yoshua akayaokoa maisha yao. Rahabu akaishi kati ya Waisraeli mpaka leo, kwa sababu aliwaficha wajumbe ambao Yoshua aliwatuma kwenda kuupeleleza muji wa Yeriko.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite