Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 19:51 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

51 Basi, kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, pamoja na viongozi wa makabila ya Waisraeli waligawanya sehemu hizo kwa kura mbele ya Yawe kwenye mulango wa hema ya kusanyiko kule Shilo. Basi, wakakamilisha kuigawanya inchi.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 19:51
18 Referans Kwoze  

Kule Shilo, Yoshua akazipigia kura sehemu hizo mbele ya Yawe, akawagawanyia Waisraeli; kila kabila na sehemu yake.


Haya ndiyo maeneo ya inchi ambayo Waisraeli walipewa katika inchi ya Kanana. Kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, pamoja na wakubwa wa ukoo za makabila ya Waisraeli waliyowagawanyia Waisraeli.


Nyuma ya kuishinda ile inchi, Waisraeli wote pamoja wakakusanyika kule Shilo na kulisimika hema la kusanyiko.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.


Na Yesu akawaambia: “Hakika mutaubeba muzigo nitakaoubeba. Lakini kuikalisha mutu kwa upande wangu wa kuume au wa kushoto si kazi yangu. Ni Mungu peke yake atakayeweka watu aliowatayarisha kwenye nafasi zile.”


Aliacha makao yake kule Shilo, makao ambamo alikaa kati ya watu.


Kila mwaka Elekana alisafiri kutoka Rama kwenda kuabudu na kumutolea Yawe wa majeshi sadaka kule Shilo. Kule, wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi, walikuwa makuhani wa Yawe.


Mukuwe macho. Wabinti wa Shilo watakapotoka inje kwa kucheza wakati wa sikukuu, mutoke kwenye mizabibu na kila mutu ajikamatie binti mumoja akuwe muke wake. Kisha murudi katika inchi ya Benjamina.


Basi wakakumbuka kwamba sikukuu ya Yawe iliyofanyika kila mwaka kule Shilo, muji unaokuwa upande wa kaskazini wa Beteli, kwenye njia kubwa inayotoka Beteli kwenda Sekemu, ilikuwa inakaribia.


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Naye alipokwisha kuteketeza mataifa saba yaliyokaa katika inchi ya Kanana, akatoa inchi ile kwa lile taifa lake kuwa urizi wao.


Kisha Yawe akamwambia Yoshua,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite