Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 18:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Basi, watu hao wakaanza safari ya kwenda kuichunguza inchi. Mbele hawajakwenda, Yoshua akawapa maagizo: “Muende katika inchi yote muandike maelezo kamili juu ya hiyo inchi, kisha murudie kunielezea, nami nitapiga kura mbele ya Yawe hapahapa Shilo juu ya sehemu mutakayopewa.”

Gade chapit la Kopi




Yoshua 18:8
13 Referans Kwoze  

Basi kwa hiyo tujikaze sana kufanya mambo yale yanayoleta amani na yanayotusaidia kujengana katika imani.


Kule Shilo, Yoshua akazipigia kura sehemu hizo mbele ya Yawe, akawagawanyia Waisraeli; kila kabila na sehemu yake.


Saulo akasema: “Ee Yawe wa Israeli, kwa nini haujanijibu mimi mutumishi wako? Ee Yawe wa Israeli, ikiwa kosa liko kwangu au kwa Yonatani mwana wangu, basi, jiwe la Urimu lionekane. Lakini ikiwa kosa hilo liko kwa watu wako Waisraeli, jiwe la Tumimu lionekane.” Yonatani na Saulo walipatikana kuwa na kosa, lakini watu walionekana hawana kosa.


Mutayarishe maelezo kamili juu ya sehemu zote saba na kuniletea. Hapo, nitapiga kura mbele ya Yawe, Mungu wetu, juu ya sehemu ya kila kabila lenu.


Nyuma ya kuishinda ile inchi, Waisraeli wote pamoja wakakusanyika kule Shilo na kulisimika hema la kusanyiko.


Eneo la inchi watu wa kabila la Yuda walilopewa kwa kura kulingana na jamaa zake lilienea tangu kusini mashariki mpaka kwa mupaka wa Edomu. Sehemu ya kusini kabisa ilikuwa jangwa la Sini.


Utayagawanyia inchi hizo makabila kenda na nusu ya kabila la Manase ambao bado hawajapata kitu.”


Basi, simama uitembelee inchi hii katika upana na urefu, maana nitakupa wewe inchi ile.”


Wanaume hao wakazunguka katika inchi yote, wakachapa taswira kamili juu ya sehemu zake saba pamoja na miji yake, kisha wakarudi kwa Yoshua kule katika kambi Shilo.


Yawe amepanga sehemu ya kila mumoja wao, ametumia kamba kuwapimia inchi hiyo; watairizi milele na milele, wataishi mule kizazi hata kizazi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite