Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 18:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kule Shilo, Yoshua akazipigia kura sehemu hizo mbele ya Yawe, akawagawanyia Waisraeli; kila kabila na sehemu yake.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 18:10
24 Referans Kwoze  

mumushukuru Mungu Baba aliyewawezesha ninyi kuwa wenye kustahili kupokea sehemu yenu ya urizi aliowawekea watu wake katika ufalme wa mwangaza.


Naye alipokwisha kuteketeza mataifa saba yaliyokaa katika inchi ya Kanana, akatoa inchi ile kwa lile taifa lake kuwa urizi wao.


Mutayarishe maelezo kamili juu ya sehemu zote saba na kuniletea. Hapo, nitapiga kura mbele ya Yawe, Mungu wetu, juu ya sehemu ya kila kabila lenu.


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Nao walipokwisha kumutundika juu ya musalaba, wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Hilo ndilo eneo la makabila ya Waisraeli. Humo ndimo watapewa maeneo yao, kila kabila eneo lake. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Mutaigawanya kuwa mali yenu. Wageni watakaokaa kati yenu, wale watakaozalia watoto kati yenu, wapewe vilevile sehemu ya inchi munapoigawanya. Hao wanapaswa kutendewa kama wanainchi wa Israeli na wana haki ya kupiga kura kwa kupata sehemu ya inchi pamoja na makabila ya Waisraeli.


Kura inakomesha ubishi; inaamua kati ya wakubwa wanaopingana.


Ninaomba nikae katika nyumba yako milele, nipate kukimbilia chini ya mabawa yako.


Ametuwezesha kuwashinda watu wa mataifa, ameyaweka mataifa chini ya mamlaka yetu.


Basi, kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, pamoja na viongozi wa makabila ya Waisraeli waligawanya sehemu hizo kwa kura mbele ya Yawe kwenye mulango wa hema ya kusanyiko kule Shilo. Basi, wakakamilisha kuigawanya inchi.


Basi, watu hao wakaanza safari ya kwenda kuichunguza inchi. Mbele hawajakwenda, Yoshua akawapa maagizo: “Muende katika inchi yote muandike maelezo kamili juu ya hiyo inchi, kisha murudie kunielezea, nami nitapiga kura mbele ya Yawe hapahapa Shilo juu ya sehemu mutakayopewa.”


Yawe akamwambia Musa:


Wanaume hao wakazunguka katika inchi yote, wakachapa taswira kamili juu ya sehemu zake saba pamoja na miji yake, kisha wakarudi kwa Yoshua kule katika kambi Shilo.


Kura ya kwanza ililipata kabila la Benjamina kulingana na ukoo zake. Eneo walilopewa watu hao lilikuwa katikati ya lile la kabila la Yuda na lile la kabila la Yosefu.


Muende kwenye pahali pangu kule Shilo, nafasi nilipochagua kwa kuabudiwa mara ya kwanza, muone maangamizi niliyofanya kule kwa sababu ya uovu wa watu wangu, Israeli.


Kwa hiyo hamutagawanyiwa sehemu yoyote ya inchi kati ya watu wa Yawe.


Sehemu hiyo yao waligawanyiwa kwa kura kama vile Yawe alivyomwamuru Musa awape yale makabila tisa na nusu.


Basi, Waisraeli wakaigawanya inchi kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Inchi za mataifa yaliyobaki na yale niliyoyaangamiza nimewagawanyia zikuwe mali ya makabila yenu, kutoka Yordani mpaka bahari ya Mediteranea, upande wa magaribi.


Waligawanywa kwa kupiga kura maana kulikuwa wakubwa wa Pahali Patakatifu na viongozi wa Mungu kati ya ukoo zote mbili; ukoo wa Eleazari na ukoo wa Itamari.


Kisha, viongozi wa watu wakakaa katika Yerusalema; watu wengine wote, wakapiga kura kati ya kila jamaa kumi kwa kuchagua jamaa moja itakayokaa katika Yerusalema, muji mutakatifu. Jamaa zingine tisa zikakaa katika miji yao mingine.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite