Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 15:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kutoka hapo, ulielekea kwenye mulima mpaka chemichemi za Nefutoa, mpaka kwenye miji ya mulima wa Efuroni. Hapo mupaka uligeuka na kuelekea Bala, ni kusema Kiriati-Yearimu,

Gade chapit la Kopi




Yoshua 15:9
8 Referans Kwoze  

Daudi akiandamana na Waisraeli wote, akaenda mpaka katika muji wa Bala, ni kusema Kiriati-Yearimu, katika inchi ya Yudea, kwa kulitwaa toka kule Sanduku la Agano linaloitwa kwa jina la Yawe anayeikaa kwenye kiti chake cha kifalme juu ya makerubi.


Upande wa kusini mupaka wake ulianzia Kiriati-Yearimu, ukafika Efuroni na kwenda mpaka kwenye chemichemi ya maji ya Nefutoa.


wakaenda kupiga kambi yao kule Kiriati-Yearimu katika inchi ya Yuda. Ndiyo maana pahali pale, upande wa magaribi wa Kiriati-Yearimu pameitwa Kambi ya Dani mpaka leo.


Daudi aliondoka pamoja nao wote kuenda Bali-Yuda kwa kuleta Sanduku la Mungu linaloitwa kwa jina la Yawe wa majeshi, anayeikaa kwenye kiti chake cha kifalme juu ya makerubi.


Basi, Waisraeli wakafunga safari, nyuma ya siku ya tatu wakafika katika miji yao. Miji hiyo ilikuwa Gibeoni, Kefira, Beroti na Kiriati-Yearimu.


Walituma wajumbe kwenda kwa wakaaji wa muji wa Kiriati-Yearimu, waseme: “Wafilistini wamelirudisha Sanduku la Yawe, mukuje mulikamate.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite