Yoshua 14:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Siku hiyo Musa akaniapia: ‘Hakika sehemu ya inchi ile ambayo ulipita ndani yake itakuwa yako wewe na wazao wako milele. Kwa sababu ya uaminifu wako kwa Yawe, Mungu wako’.
Kalebu mwana wa Yefune, ndiye tu atakayeiona. Nami nitamupatia inchi hiyo aliyokanyaga ndani ikuwe yake yeye na wazao wake kwa sababu amekuwa mwaminifu kabisa kwangu.’
Wakakwenda mpaka Negebu wakapita mpaka muji wa Hebroni. Humo wakawakuta Waahimani, Wasesai na Watalmai, wazao wa Anaki. (Muji wa Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba mbele ya muji wa Soani unaokuwa katika inchi ya Misri).
Kila pahali mutakapokanyaga kwa miguu yenu patakuwa penu. Inchi yenu itaenea kutoka katika jangwa, upande wa kusini, mpaka kwenye milima ya Lebanoni upande wa kaskazini, na kutoka muto Furati upande wa mashariki, mpaka kwenye bahari ya Mediteranea upande wa magaribi.
Lakini sasa ni muda wa miaka makumi ine na mitano tangu Yawe aliposema na Musa, wakati Waisraeli walipokuwa wanapita katika jangwa. Tangu wakati ule Yawe, kama vile alivyoahidi, amenilinda muzima mpaka leo, na sasa mimi nina umri wa miaka makumi nane na mitano.