Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 14:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Sasa ninaomba unipe inchi hii ya milima ambayo Yawe aliniahidi siku ile. Wewe ulisikia siku ile kwamba Waanaki waliishi humo katika miji yenye kuta; labda Yawe atakuwa pamoja nami, nami nitawafukuza kama vile Yawe alivyosema.”

Gade chapit la Kopi




Yoshua 14:12
21 Referans Kwoze  

Kwa njia ya imani hawa walishinda inchi za wafalme, walitenda mambo ya haki na kupata yale Mungu aliyowaahidi. Walifunga vinywa vya simba,


Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.


Tuliona majitu huko, wazao wa Anaki. Sisi tulijiona kuwa kama mapanzi mbele yao, na ndivyo walivyotuona sisi.


Lakini wenyeji wake ni wenye nguvu sana, na miji yao ni imara na mikubwa sana. Zaidi ya hayo, huko tuliona wazao wa Anaki.


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Kalebu alizifukuza kutoka muji huo ukoo tatu za Anaki, ni kusema ukoo wa Sesayi, ukoo wa Ahimani na ukoo wa Talmayi.


Si wewe Mungu ambaye umetutupilia? Lakini hauendi tena na jeshi letu.


Kwa mukono wako mwenyewe uliyafukuza mataifa, na mahali pao ukawaikalisha watu wako; uliyaazibu mataifa, na kuwafanikisha watu wako.


Yawe akawashinda Waetiopia mbele ya Asa na jeshi lake la watu wa Yuda. Waetiopia wakakimbia.


Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”


Muji wa Hebroni ukapewa kwa Kalebu kufuatana na maagizo ya Musa. Kalebu akazifukuza kutoka kule ukoo tatu za Anaki.


Lakini Yawe akamwambia Musa: Usimwogope, maana nimemutia katika mikono yako pamoja na watu wake wote na inchi yake yote. Utamutendea kama ulivyomutendea Sihoni, mufalme wa Waamori, aliyekuwa anakaa Hesiboni.


Kwa nini tuende huko wakati tumevunjika moyo kwa hofu? Wametuambia kwamba watu wa huko ni wakubwa na warefu kuliko sisi, na kwamba miji yao ni mikubwa na yenye kuta zinazofika katika mawingu. Tena wamesema kwamba waliwaona wale wazao wa Anaki!’


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyosikia. Uwaombee watu wanaobaki.’ ”


“Musikilize enyi Waisraeli! Hivi leo mumekaribia kuvuka muto Yordani, kwenda kurizi inchi ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi. Miji yao ni mikubwa na ina kuta zinazofika katika mawingu.


Mujue leo hii kwamba anayewatangulia kama vile moto unaoteketeza miti ni Yawe, Mungu wenu. Atawaangamiza na kuwashinda mbele yenu, kwa hiyo mutawafukuza na kuwaangamiza mara moja, kama vile Yawe alivyowaahidi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite